Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Nehemia 2:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Nikamujibu: “Ee mufalme, ikikupendeza, ninaomba nipewe barua kusudi nizipeleke kwa watawala wa jimbo la upande wa magaribi wa muto Furati kusudi waniruhusu nipite mpaka katika inchi ya Yuda.

Gade chapit la Kopi




Nehemia 2:7
6 Referans Kwoze  

Mimi mufalme Artasasta, ninatoa amri kwa walinzi wa hazina wote katika jimbo la upande wa magaribi wa muto Furati kwamba kitu chochote Ezra atakachohitaji, kuhani na mwandishi wa Sheria ya Mungu wa mbinguni, mutamupa, tena bila kusita,


Nilipowafikia wakubwa wa jimbo la upande wa magaribi wa muto Furati, nikawapa barua za mufalme. Mufalme alikuwa amenituma pamoja na wakubwa wa waaskari na waaskari wapanda-farasi.


Vilevile wakawapa wasimamizi wa mufalme na watawala wa mukoa wa majimbo ya upande wa magaribi wa muto Furati maagizo waliyopewa na mufalme, nao wakatoa musaada kwa watu na kwa ajili ya nyumba ya Mungu.


Halafu Dario akatuma ujumbe huu: Kwa Tatenayi, mutawala wa jimbo la upande wa magaribi wa muto Furati, Setari-Bozenayi na wakubwa wenzako katika jimbo. Musiende kule kwenye hekalu,


Ingekuwa haya kubwa kwangu kumwomba mufalme kundi la waaskari na waaskari wapanda-farasi wa kutulinda na waadui katika njia maana nilikuwa nimekwisha kumwambia kwamba Mungu wetu anawabariki wote wanaomutafuta, lakini anawachukia na kuwaazibu wote wanaomwacha.


Waliowafuata hao katika kazi hiyo ya kujenga upya walikuwa Melatia, Mugibeoni; Yadoni, Mumeronoti pamoja na watu wa muji wa Gibeoni na Misipa waliokuwa chini ya uongozi wa mutawala wa jimbo la upande wa magaribi wa muto Furati.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite