Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Nehemia 10:29 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

29 Sisi wote, watu wa Israeli, makuhani, Walawi, walinzi wa milango, waimbaji, watumishi wa hekalu na watu wote waliojitenga na mataifa jirani kufuata sheria ya Mungu pamoja na wake zao, wana wao, na wabinti zao, wote wenye maarifa na ufahamu,

Gade chapit la Kopi




Nehemia 10:29
38 Referans Kwoze  

Nitatia roho yangu ndani yenu; nitawafanya mufuate masharti yangu na kushika maagizo yangu.


Nimeapa na kuhakikisha kiapo changu, kwamba nitashika maamuzi yako ya haki.


Ninyi ni warafiki zangu, kama mukifanya sawa ninavyowaagiza.


Upendo wenu ukuwe pasipo udanganyifu. Muchukie chochote kinachokuwa kibaya, mushikamane na kinachokuwa chema.


Kisha mufalme akasimama kwa pahali pake akafanya agano mbele ya Yawe, kumufuata Yawe, kushika amri, maamuzi na masharti yake kwa moyo wake wote na kwa roho yake yote, kutenda maneno yote ya agano yaliyoandikwa katika kitabu hiki.


Halafu mufalme akasimama karibu na nguzo na kufanya agano mbele ya Yawe, kumufuata Yawe, kushika amri zake, maagizo na masharti yake kwa moyo wake wote na kwa roho yake yote, kutenda maneno yote ya agano yaliyoandikwa katika kitabu hicho; nao watu wote wakaungana katika kufanya agano.


Lakini wewe usikubali ombi lao, kwa sababu kuna watu zaidi ya makumi ine wanaovizia kumwua. Watu hawa wamefanya kiapo kwamba hawatakula wala kunywa mpaka wamwue Paulo kwanza.”


Ingawa vile watu wamoja walijiunga naye na kuamini. Kati yao kulikuwa Dionisio, mumoja wa Baraza Kubwa inayoitwa Areopago, pamoja na mwanamuke mumoja aliyeitwa Damari na watu wengine vilevile.


Naye alipofika, akaona mambo yote yaliyotendeka kutokana na neema ya Mungu, akafurahi, naye akawatia wanafunzi wote moyo kusudi waendelee kushikamana na Bwana kwa moyo wao wote.


Musa hakuwapa ninyi Sheria? Ingawa hivyo hakuna mumoja wenu anayetii Sheria. Na sasa sababu gani munatafuta kuniua?”


Sheria ya Mungu ilitolewa kwa njia ya Musa, lakini neema na ukweli vilikuja kwa njia ya Yesu Kristo.


Utawaambia kwamba: Yawe anasema hivi: Kama hamutanisikiliza na kufuata sheria zangu nilizowawekea,


Yawe atawahurumia tena watu wa Yakobo, atawachagua tena Waisraeli. Atawarudisha katika inchi yao wenyewe, na wageni watakuja na kukaa pamoja na watu wa Yakobo.


kusudi watu wake watii masharti yake, na kufuata sheria zake. Haleluia!


ndege, samaki, na viumbe vyote vya bahari.


Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa mutindo wa watu wa Gati. Zaburi ya Daudi.


Nikawakaripia na kuwalaani, hata nikawapiga wamoja kati yao na kuwaongoa nywele zao. Nikawalazimisha kuapa kwa jina la Mungu, nikisema: “Wabinti zenu musiwaoeshe kwa vijana wao, wala wabinti zao wasiolewe na vijana wenu au na ninyi wenyewe.


“Kwa hiyo sasa, Ee Yawe, Mungu wa Israeli, ninakuomba tena utimize ile ahadi uliyomwahidi mutumishi wako Daudi baba yangu, ukisema: ‘Siku zote utakuwa na mutu wa uzao wako wa kuikaa katika kiti cha kifalme cha Israeli, ikiwa wazao wako wataangalia mwenendo na kushika sheria zangu kama vile wewe ulivyofanya mbele yangu.’


Lakini Yehu hakutii sheria za Yawe, Mungu wa Israeli, kwa moyo wake wote. Hakuacha zambi zile za Yeroboamu ambaye aliwasukuma watu wa Israeli watende zambi.


Musa alituamuru tutii sheria; ni mali ya taifa letu.


“Ninyi mukuwe waangalifu mufanye kama vile Yawe alivyowaamuru. Mutimize kila kitu sawasawa.


Musa akawaita pamoja Waisraeli, akawaambia: “Enyi Waisraeli, musikilize masharti na maagizo ambayo ninayasema mbele yenu leo. Mujifunze hayo na kuyatimiza kwa uangalifu.


Yawe akuazibu hata ukuwe laana na kiapo kati ya watu wako, ukuwe tasa na tumbo lako livimbe.


Hivi karibu siku hizi ninyi mulibadilika, mukafanya mambo yanayokuwa sawa mbele yangu, mukawaachilia huru Waisraeli wenzenu na kufanya agano mbele yangu katika nyumba yangu.


Kwa sababu mimi Yawe ni mutakatifu, nami nimewatenga ninyi na mataifa mengine kusudi mukuwe mali yangu, mutakuwa watakatifu.


Watu wa kwanza kurudia katika miji ya inchi yao walikuwa Waisraeli wa kawaida, makuhani, Walawi na watumishi wa hekalu.


Ukoo za watumishi wa hekalu waliorudi kutoka katika uhamisho zilikuwa ukoo za: Siha, Hasufa, Tabaoti, Kerosi, Siaha, Padoni, Lebana, Hagaba, Salmai, Hanani, Gideli, Gahari, Reaya, Resini, Nekoda, Gazamu, Uza, Pasea, Besayi, Munimu, Nefusesimu, Bakibuki, Hakufa, Harihuri, Basiliti, Mehida, Harsa, Barkosi, Sisera, Tema, Nezia, Hatifa.


Ezra, ambaye alikuwa kuhani, akaenda na kuleta kitabu cha Sheria ya Musa mbele ya mukutano wote, wanaume na wanawake na yeyote aliyeweza kuelewa ile sheria. Siku hiyo ilikuwa ni siku ya kwanza ya mwezi wa saba.


Kisha Ezra akawasomea watu wote wanaume na wanawake na yeyote aliyeweza kuelewa Sheria ya Musa akiwa mbele ya Mulango wa Maji tangu asubui mpaka saa sita za muchana. Watu wote wakatega masikio yao na kusikiliza kwa uangalifu kitabu cha Sheria.


Wakati ule, walikuwa wamejitenga mbali na watu wa mataifa mengine, wakasimama na kuungama zambi zao na maovu ya babu zao.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite