Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Nehemia 1:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Tumetenda mabaya mbele yako, hatujashika amri zako, masharti na maagizo yako uliyomwagiza mutumishi wako Musa.

Gade chapit la Kopi




Nehemia 1:7
24 Referans Kwoze  

Waisraeli wote wameiasi sheria yako, wamekuacha wakakataa kukutii. Kwa sababu tumekukosea, tumemwangiwa laana na viapo vilivyoandikwa katika Sheria ya Musa, mutumishi wako.


Umetuazibu kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Musa, lakini mpaka sasa, ee Yawe, Mungu wetu, hatukuomba musamaha wako kwa kuziacha zambi zetu na kutambua uaminifu wako.


Tumetenda zambi sisi na babu zetu; tumetenda maovu, tumefanya mabaya.


Hukumu zake ni za kweli na za haki. Amehukumu yule kahaba mukubwa ambaye alikuwa akipotosha dunia kwa vitendo vyake vya uasherati. Mungu amemulipiza kisasi cha damu ya watumishi wake!”


Nilisema: Hakika katika muji huu watanitii na kukubali kuonywa; hawataacha kukumbuka mara hizo zote nilizowaazibu. Lakini watu wake walizidisha tamaa zao za kufanya matendo yao kuwa upotovu.


Ninyi mumezama katika uovu, kama ilivyokuwa kule Gibea. Mungu atayakumbuka makosa yao, na kuwaazibu kwa ajili ya zambi zao.


Ezra akaondoka Babeli, yeye alikuwa mwandishi mwenye ujuzi mwingi sana katika Sheria ambayo Yawe, Mungu wa Israeli, alikuwa amemupatia Musa. Na kwa musaada wa Yawe, Mungu wake, mufalme alimupatia Ezra kila kitu alichohitaji.


Alitenda kwa usawa mbele ya Yawe kama vile Uzia baba yake alivyotenda. Hakuingia katika hekalu la Yawe. Watu waliendelea kufanya maovu.


Lakini hakuwaua watoto wao, kama vile ilivyoandikwa katika sheria zinazokuwa katika kitabu cha Musa, ambamo Yawe anatoa amri akisema: “Wazazi hawatauawa kwa ajili ya watoto wao, wala watoto hawatauawa kwa ajili ya wazazi wao; lakini kila mutu atauawa kwa ajili ya zambi zake mwenyewe.”


Timiza maagizo ya Yawe, Mungu wako, ufuate njia zake na kushika masharti yake, amri zake, maagizo yake na maamuzi yake kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Musa. Kwa hiyo, utafanikiwa katika kila jambo unalofanya na kokote unakoenda.


“Hii ndiyo amri, masharti na maagizo ambayo Yawe, Mungu wenu, aliniamuru niwafundishe, kusudi muyatimize katika inchi munayokwenda kuirizi.


Musa akawaita pamoja Waisraeli, akawaambia: “Enyi Waisraeli, musikilize masharti na maagizo ambayo ninayasema mbele yenu leo. Mujifunze hayo na kuyatimiza kwa uangalifu.


“Muangalie! Nimewafundisha masharti na maagizo kama vile Yawe, Mungu wangu alivyoniamuru nifanye, kusudi muyashike katika inchi munayokwenda kuirizi.


Musa akaendelea kusema: “Mushike basi na kufuata masharti na maagizo niliyowafundisha, kusudi mupate kuishi na kurizi inchi ambayo Yawe, Mungu wa babu zenu, anawapa.


Hizo ndizo amri ambazo Yawe alimwamuru Musa kusudi awaambie Waisraeli kwenye mulima Sinai.


Ole kwako wewe taifa lenye zambi, watu waliolemewa na uovu, kizazi cha watenda mabaya, watoto wanaoishi kwa udanganyifu! Ninyi mumemwacha Yawe, mumemuzarau Mutakatifu wa Israeli, mumerudi nyuma.


“Lakini wazao wake wakiiacha sheria yangu, wasipoishi kufuatana na maagizo yangu,


kama wakivunja masharti yangu, na kuacha kutii amri zangu,


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite