Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Nahumu 2:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Yawe anamurudishia Yakobo utukufu wake, anawapa tena Waisraeli utukufu wao, ingawa washambulizi hawakuwaachia kitu, hata matawi yao ya mizabibu waliyakata.

Gade chapit la Kopi




Nahumu 2:3
13 Referans Kwoze  

Kisha kukaonekana kitambulisho kingine mbinguni. Kulikuwa nyoka mukubwa mwekundu mwenye vichwa saba na pembe kumi. Juu ya kila kichwa kulikuwa taji saba.


Kisha kukatokea farasi mwengine mwekundu. Na yule aliyepanda juu yake akapewa uwezo wa kuondoa amani katika dunia, kusudi watu wauane wao kwa wao. Naye akapewa upanga mukubwa.


Muomboleze, enyi misunobari, kwa sababu mierezi imeteketea. Miti hiyo mitukufu imeharibiwa! Enyi mialo ya Basani, muomboleze, kwa maana pori kubwa limekatwa!


Gari la kwanza lilikokotwa na farasi wekundu, la pili lilikokotwa na farasi weusi,


Wakati wa usiku, nilimwona malaika akipanda juu ya farasi mwekundu. Malaika yule alikuwa akisimama katika bonde, katikati ya miti ya mihadasi. Nyuma yake kulikuwa farasi wengine wekundu, wa kijivujivu na weupe.


Miti ya shindano inafurahia kuanguka kwako, nayo mierezi ya Lebanoni pamoja inasema: Kwa vile sasa umeangushwa, hakuna mukata miti atakayekuja juu yetu!


Silaha wapanda-farasi wanazobeba, zinagongana kwa sauti na kuangaa kwenye jua.


Watakuja kutoka upande wa kaskazini, pamoja na magari ya vita na ya mizigo, wakiongoza kundi kubwa la watu. Watakuzunguka pande zote kwa ngao kubwa na ndogo na kofia za chuma. Nimewapa uwezo wa kukuhukumu, nao watakuhukumu kadiri ya sheria zao.


Bwana wetu Yawe anasema hivi: Kutoka upande wa kaskazini nitamuleta Nebukadneza, mufalme wa Babeli, mufalme wa wafalme, akiwa na farasi, magari ya vita, waaskari wapanda-farasi na kundi kubwa, akuje kukushambulia.


Sikia! Mulio wa fimbo, mashindo ya magurudumu, vishindo vya farasi na ngurumo za magari ya vita!


Mbona ulibomoa kuta zilizouzunguka? Sasa kila anayepita anachuma zabibu zake;


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite