Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Nahumu 2:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Enyi watu wa Yuda muangalie: Mutu anakuja kutoka milima anayeleta habari njema, anayetangaza amani. Mufanye sikukuu zenu, mutimize viapo vyenu, maana waovu hawatawashambulia, kwa sababu wameangamizwa kabisa.

Gade chapit la Kopi




Nahumu 2:1
14 Referans Kwoze  

Lakini ukitaka kwenda, basi ufanye vile, ukuwe hodari katika vita, lakini Mungu atakufanya ushindwe na waadui, kwa maana Mungu ana nguvu kwa kusaidia au kumufanya mutu ashindwe.”


Jinsi gani huo muji uliokuwa nyundo iliyoponda dunia nzima unavyoangushwa chini na kuvunjika! Babeli umekuwa pori tupu kati ya mataifa!


ambayo walipiga nayo watu kwa hasira bila kukoma, na kuwatawala kwa kuwatesa bila huruma.


basi, nitayaita makabila yote ya kaskazini pamoja na mutumishi wangu Nebukadneza, mufalme wa Babeli. –Ni ujumbe wa Yawe.– Nitawaleta waishambulie inchi hii na wakaaji wake pamoja na mataifa yote jirani. Nitawaangamiza kabisa, na kuwafanya kuwa kitu cha kuchukiza, cha kuzomewa na kuzarauliwa milele.


Shukrani ikuwe ndiyo sadaka yako kwa Mungu. Umutimizie Mungu Mukubwa ahadi zako.


Ee Mungu, unastahili sifa huko Sayuni. Watu wanapaswa kukutimizia viapo vyao,


Halafu, kundi la mataifa yote yanayoshambulia Yerusalema, wote wanaoshambulia ukuta wake na kuutia wasiwasi, watatoweka kama ndoto, kama maono ya usiku.


Mataifa yote yanayoshambulia Yerusalema yatakuwa kama mutu mwenye njaa anayeota ndoto kwamba anakula lakini anaamuka angali bado na njaa, na kama mutu mwenye kiu anayeota kwamba anakunywa lakini anaamuka muzaifu, na angali bado na kiu.


Ni furaha kabisa! Mujumbe anatokea kwenye mulima. Anatangaza habari njema za amani, heri, na ukombozi. Anauambia Sayuni: Mungu wako anatawala!


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite