Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Nahumu 1:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Waadui wakishambulia inchi kama mafuriko, yeye anawaangamiza; anawafuatilia na kuwafukuza mpaka katika giza.

Gade chapit la Kopi




Nahumu 1:8
26 Referans Kwoze  

Kwa hiyo Bwana wetu Yawe anasema: Kwa kasirani yangu nitazusha upepo wa zoruba na mvua nyingi ya mawe, navyo vitauangusha ukuta huo.


Nitatumia sheria kama kipimo changu, nitatumia haki kama timazi. Mvua ya mawe itaufagilia mbali uongo munaoutegemea, na mafuriko yataharibu kikingio chenu.


na kuiangalia dunia, lakini wataona tu taabu, giza na mateso makubwa. Hakuna atakayeepuka giza hilo kubwa.


Yawe atanyoosha mukono wake kwa kuazibu inchi ya upande wa kaskazini, na kuiangamiza inchi ya Asuria. Ataufanya muji wa Ninawe kuwa ukiwa, kuwa pahali penye kukauka kama jangwa.


Kwa hiyo, dunia itatetemeka na kila mutu katika inchi atafanya kilio. Inchi yote itayumbayumba; itapanda na kushuka, kama vile maji ya muto Nili yanavyojaa na kupunguka!


Lakini wale waliopaswa kushiriki katika Ufalme ule watatupwa inje kwenye giza, na kule watalia na kusaga meno.”


Mvua ikanyesha, mito ikajaa, upepo ukavuma na kupiga nyumba ile, nayo ikaanguka na kubomoka kabisa.”


Muji uko wazi kabisa, watu wamekamatwa mateka. Wanawake wake wanaomboleza, wanalia kama njiwa, na kujipigapiga kwenye vifua.


Ujumbe wa Mungu juu ya Ninawe. Kitabu cha maono ya Nahumu wa Elkosi.


Wakati wa mwisho mufalme wa kusini atamushambulia mufalme huyo wa kaskazini. Lakini mufalme wa kaskazini atajibu mashambulio hayo kwa nguvu kama zoruba, akitumia magari ya vita, waaskari wapanda-farasi na mashua nyingi. Atashambulia inchi nyingi na kupita katika inchi hizo kama mafuriko ya maji.


Makundi ya waaskari pamoja na kuhani wa hekalu wataangamizwa na kuwaua.


Kisha majuma hayo makumi saba na mawili, yule aliyepakwa mafuta atauawa na hatabaki na kitu. Muji na Pahali Patakatifu Sana vitaharibishwa na waaskari wa mutawala atakayekuja kushambulia. Mwisho wake utafika kama mafuriko, kukiwa vita na maangamizi kama yalivyopangwa na Mungu.


Mumutukuze Yawe, Mungu wenu, mbele hajawaletea giza, mbele hamujajikwaa miguu kwenye milima inayofunikwa na giza. Ninyi mulitazamia mwangaza, lakini anaugeuza kuwa usiku anaufanya kuwa giza nzito.


Lakini njia ya waovu ni kama giza nene, hawajui kinachowafanya wajikwae.


Hofu kubwa imenishika. Heshima yangu imetoweka kama kwa upepo, na raha yangu imepita kama wingu.


Wana wa mufalme wa kaskazini watakusanya kundi kubwa la waaskari na kujitayarisha kwa vita. Kundi hilo litasonga mbele kama mafuriko ya maji litapita na kupigana vita mpaka ndani ya muji wenye kuta wa waadui.


Uwamwangie watu hasira yako kubwa; umwangalie kila mwenye kiburi na kumwangusha.


Siku ya Yawe inakuja, siku kali, ya kasirani na hasira kali. Itaifanya inchi kuwa uharibifu, itawaangamiza wenye zambi ndani yake.


Nyota na vikundi vyake katika anga hazitaangaza; jua linapochomoza litakuwa giza, na mwezi hautatoa mwangaza wake.


Bwana amejichagulia mutu wake shujaa na mwenye nguvu, ambaye ni kama mvua ya mawe na zoruba kali, kama zoruba ya mafuriko makubwa; kwa mukono wake atawatupa chini.


Hivi ndivyo Babeli utakavyozama, wala hautainuka tena, kwa sababu ya hasara ambayo Yawe anauletea. Huu ndio mwisho wa maneno ya Yeremia.


Anayalinda maisha ya waaminifu wake, lakini anaangamiza maisha ya waovu katika giza. Maana, mwanadamu hapati ushindi kwa nguvu zake.


Halafu agano lenu na kifo litavunjika, na mapatano yenu na kuzimu yatafutwa. Ile hasara kubwa itakapokuja itawaangusha chini.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite