Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Nahumu 1:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Nani anayeweza kusimama mbele ya kasirani ya Yawe? Nani anayeweza kuvumilia ukali wa hasira yake? Yeye anaimwanga hasira yake inayowaka kama moto, hata mawe makubwa anayapasua vipandevipande.

Gade chapit la Kopi




Nahumu 1:6
31 Referans Kwoze  

Lakini Yawe ni Mungu wa kweli, Mungu Mwenye Uzima, mufalme wa milele. Akikasirika, dunia inatetemeka, mataifa hayawezi kuvumilia hasira yake.


Lakini ni nani atakayevumilia siku ile atakapokuja? Ni nani atakayesimama kuvumilia atakapotokea? Yeye ni kama moto mukali unaosafisha chuma; ni kama sabuni ya mwenye kufua nguo.


Yawe ni Mungu mwenye wivu, anayelipiza kisasi; Yawe analipiza kisasi na ni mwenye kasirani; Yawe analipiza kisasi kwa wapinzani wake, kasirani yake inawaka juu ya waadui zake.


Ulipowakaripia, ee Mungu wa Yakobo, farasi na wapanda-farasi walipooza.


Nitateketeza inchi ya Misri kwa moto. Sini utashikwa na wasiwasi mukubwa, ukuta wa Nofi utabomolewa, nao Nofi utashambuliwa na waadui muchana wazi.


Yawe ameonyesha kabisa kasirani yake, aliimwanga hasira yake kali, aliwasha moto huko katika Sayuni ambao uliteketeza misingi yake.


Amevuta upinde wake kama adui, na kuuweka mukono wake wa kuume tayari, amewaua wote waliopendeza macho. Amemwanga hasira yake kama moto katika hema yetu watu wa Sayuni.


Silikasirikii tena shamba hili; kama miiba na michongoma ingelilishambulia, mimi ningepambana nayo na kuichoma kwa moto.


Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe wa majeshi, atawaletea waaskari wao wanene ugonjwa wa kuwakondesha, na utukufu wao utateketezwa kama kwa moto.


Nani anayetambua uzito wa hasira yako? Nani anayeona matokeo ya kasirani yako?


Yawe akamwambia: “Kwenda usimame juu ya mulima, mbele yangu mimi Yawe.” Basi, Yawe akapita na kuuvumisha upepo mukali ambao uliporomosha milima na kuvunja mawe makubwa. Lakini Yawe hakukuwa katika upepo ule. Upepo ukapita, kukakuwa tetemeko la inchi. Lakini Yawe hakukuwa katika tetemeko la inchi.


Malaika wa ine akamwanga kikombe chake juu ya jua, nalo likapewa uwezo wa kuwaunguza watu kwa joto lake.


Kisha nikasikia sauti kubwa ikitoka katika hekalu ikiwaambia wale wamalaika saba: “Mwende kumwanga vile vikombe saba vya kasirani ya Mungu juu ya dunia!”


Kwa maana siku kubwa ya kasirani yao imekuja. Ni nani atakayeweza kusimama imara?”


Uwamwangie watu hasira yako kubwa; umwangalie kila mwenye kiburi na kumwangusha.


Ee Yawe, kama ungekumbuka maovu yetu, nani, ee Bwana wetu, angeweza kuishi?


Nitazitetemesha mbingu nayo inchi itatikisika katika misingi yake kwa sababu ya kasirani ya Yawe wa majeshi, siku ile ya hasira yangu kali.


Yawe atakuja kama moto, na magari yake ya vita ni kama zoruba. Ataiacha hasira yake ifanye kazi yake kwa ukali, na maonyo yake yatimizwe kwa ndimi za moto.


Enyi jamaa ya Daudi, Yawe anasema hivi: Kila asubui muamue maneno kufuatana na sheria yangu, muwakomboe wote walionyanganywa mali zao toka katika mikono ya watesaji. Kama si vile, hasira yangu itawaka kama moto, wala hakuna atakayeweza kuizimisha, kwa sababu ya matendo yenu maovu.


Sasa mutausikia uzito wa hasira yangu juu yenu. Nitawahukumu kulingana na mwenendo wenu; nitawaazibu kufuatana na machukizo yenu.


Bwana wetu Yawe anasema hivi: tosha kitambulisho chako cha kifalme na taji yako, maana mambo hayatabaki kama yalivyokuwa. Wanaokuwa chini watanyanyuliwa, wanaokuwa juu watashushwa!


Nitawasha moto juu ya inchi ya Magogi na juu ya wote wanaokaa salama katika inchi za kandokando ya bahari. Nao watatambua kwamba mimi ni Yawe.


mbele hamujapeperushwa mbali kama maganda, mbele haijawafikia siku ya hasira kali ya Yawe, mbele haijawafikia siku ya kasirani ya Yawe.


Yeye anahamisha milima bila yenyewe kutambua, anaipindua mbali kwa hasira yake.


Mungu akitoa sauti ya kukaripa, nguzo za mbingu zinatetemeka na kushangaa.


Wewe, ee Mungu, ni wa kutisha sana! Nani anayeweza kusimama mbele yako ukikasirika?


Wenye zambi katika Sayuni wanaogopa, wasiomwamini Mungu wanatetemeka na kusema: Nani anayeweza kuvumilia moto huu mukali? Nani anayeweza kuvumilia ndimi za moto usiozimika?


Ameivunja kwa hasira nguvu yote ya Israeli. Hakunyoosha mukono kwa kuwasaidia walipokutana na adui; amewawakia watu wa Yakobo kama moto, akateketeza kila kitu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite