Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Nahumu 1:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Milima inatetemeka mbele yake, vilima vinayeyuka. Dunia inatetemeka mbele yake, ulimwengu na vyote vinavyokuwa ndani yake.

Gade chapit la Kopi




Nahumu 1:5
34 Referans Kwoze  

Milima itayeyuka chini ya miguu yake, kama inta karibu na moto; mabonde yatapasuka, kama vile maji yanayoporomoka kwenye muteremuko.


Niliangalia milima, nikaiona ikitetemeka, navyo vilima vyote vilikuwa vikiyumbayumba.


Halafu, dunia ikatetemeka na kutikisika, misingi ya mbinguni ikayumbayumba na kuruka, kwa maana Mungu alikuwa amekasirika.


Milima ilikuona, ikanyauka; mafuriko ya maji yakapita mule. Vilindi vya bahari vilinguruma, na kurusha juu mawimbi yake.


Ee Mungu, ulipowaongoza watu wako, uliposafiri kule katika jangwa,


Milima ilitikisika mbele yako Yawe, mulima Sinai mbele yako Yawe, Mungu wa Israeli.


Enyi milima, mbona muliruka kama kondoo dume? Nanyi vilima, namna gani mumeruka kama mwana-kondoo?


Milima ilirukaruka kama kondoo dume; vilima vikaruka kama wana-kondoo!


Bahari ivume na vyote vinavyokuwa ndani yake, dunia na wote wanaoishi ndani yake.


Mungu yuko katika muji huo, nao hauwezi kutikiswa; Mungu ataupatia musaada kila asubui.


Mulima wa Sinai ulikuwa umefunikwa na moshi kwa sababu Yawe alishuka juu yake katika moto. Moshi wa moto ule ulipanda juu kama moshi wa furu kubwa na mulima wote ukatetemeka kwa nguvu.


Kisha nikaona kiti kikubwa cheupe cha kifalme pamoja na yule aliyeikaa juu yake. Dunia na mbingu vikatoweka mbele yake navyo havikuonekana tena.


Kwa rafla kukatokea tetemeko la inchi, kwa maana malaika wa Bwana alishuka toka mbinguni, akasukuma lile jiwe lililofunga kaburi pembeni na kuikaa juu yake.


Na saa ile ile pazia la hekalu likapasuka vipande viwili toka juu mpaka chini. Inchi ikatetemeka, mawe makubwa yakapasuka,


Mbingu zikaviringwa na kuwa kama kizingo cha karatasi na kutoweka. Milima yote na visanga vyote vikahamishwa kutoka kwenye nafasi yao.


Katika taabu yangu, nilimwita Yawe; nilimulilia Mungu wangu anisaidie. Toka katika hekalu lake, alisikia sauti yangu; kilio changu kilimufikia katika masikio yake.


Kwa hiyo hasira ya Yawe iliwawakia watu wake, akaunyoosha mukono wake juu yao, akawaazibu. Milima ikatetemeka, maiti zao zikakuwa kama takataka katika barabara za muji. Hata hivyo, hasira yake haijatulia, angali ananyoosha mukono wake kwa kuwaazibu.


Sasa Yawe anaiharibu dunia na kuifanya tupu. Atavuruga uso wa dunia na kuwatawanya wakaaji wake.


Inapepesuka kama mulevi, inayumbayumba kama kibanda. Imelemewa na muzigo wa zambi zake nayo itaanguka wala haitasimama tena.


Inchi inatetemeka mbele yao, mbingu zinatikisika. Jua na mwezi vinatiwa giza, nazo nyota zinaacha kuangaza.


Tena, akaongeza kusema: Mulima huu ni kizuizi? Hapana! Wewe Zerubabeli utausawazisha. Wewe utaanzisha ujenzi mupya wa hekalu, na wakati utakapoliweka jiwe la mwisho, watu watashangilia wakisema: Ni zuri! Kweli, ni zuri!


Yeye anahamisha milima bila yenyewe kutambua, anaipindua mbali kwa hasira yake.


Mungu akitoa sauti ya kukaripa, nguzo za mbingu zinatetemeka na kushangaa.


Halafu dunia ikatetemeka na kutikisika, misingi ya milima ikayumbayumba na kutetemeka, kwa maana Mungu alikuwa amekasirika.


Anaiangalia dunia, nayo inatetemeka; anagusa milima, nayo inatoa moshi!


Lakini Yawe ni Mungu wa kweli, Mungu Mwenye Uzima, mufalme wa milele. Akikasirika, dunia inatetemeka, mataifa hayawezi kuvumilia hasira yake.


Samaki na ndege, nyama wa pori, viumbe vyote vinavyotambaa pamoja na watu wote katika dunia, watatetemeka kwa kuniona. Milima itaporomoshwa, mawe yataanguka na kuta zote zitaanguka chini.


Bwana wetu Yawe wa majeshi, anaigusa dunia nayo inatetemeka, na wakaaji wake wanaomboleza; dunia nzima inapanda na kushuka kama vile muto Nili wa Misri unavyojaa na kupunguka.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite