Nahumu 1:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
12 Yawe anasema hivi: Ingawa Waasuria ni wengi na wenye nguvu, wao wataangushwa na kuangamizwa. Ingawa nimewatesa ninyi watu wangu, sitawatesa tena zaidi.
Wana wa mufalme wa kaskazini watakusanya kundi kubwa la waaskari na kujitayarisha kwa vita. Kundi hilo litasonga mbele kama mafuriko ya maji litapita na kupigana vita mpaka ndani ya muji wenye kuta wa waadui.
Basi, malaika wa Yawe aliingia ndani ya kambi ya Waasuria na kuwaua watu elfu mia moja makumi nane na watano. Kesho yake, wakati watu walipoamuka, waliona yale maiti yote.
Hapo Waasuria watauawa kwa upanga, lakini si upanga wa watu; wataangamizwa kwa upanga ambao ni zaidi ya ule wa wanadamu. Waasuria watakimbia na vijana wao watatumikishwa kazi za kitumwa.
Enyi watu wa Sayuni, enyi watu wa Yerusalema, hakika ninyi hamutaomboleza tena. Kweli Mungu atawahurumia; mara tu atakaposikia kilio chenu atawaitikia.
Siku moja wakati Saniharibu alipokuwa akiabudu katika nyumba ya Nisiroki mungu wake, wana wake wawili, Adarameleki na Sarezeri walimwua kwa upanga, halafu wakakimbilia katika inchi ya Ararati. Halafu mwana wake Esari-Hadoni akatawala kwa pahali pake.
Basi, malaika wa Yawe aliingia ndani ya kambi ya Waasuria na kuwaua watu elfu mia moja makumi nane na watano. Kesho yake, wakati watu walipoamuka, waliona yale maiti yote.