Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Nahumu 1:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Yawe anasema hivi: Ingawa Waasuria ni wengi na wenye nguvu, wao wataangushwa na kuangamizwa. Ingawa nimewatesa ninyi watu wangu, sitawatesa tena zaidi.

Gade chapit la Kopi




Nahumu 1:12
20 Referans Kwoze  

Alisikiliza, akajibu maombi yao, akasema: Sasa nitawapa tena ngano, divai na mafuta, nanyi mutashiba navyo. Sitawafanya muzarauliwe tena na mataifa.


Nao hawatasikia njaa tena, wala kiu, wala jua halitawapiga tena, wala joto lolote.


Wana wa mufalme wa kaskazini watakusanya kundi kubwa la waaskari na kujitayarisha kwa vita. Kundi hilo litasonga mbele kama mafuriko ya maji litapita na kupigana vita mpaka ndani ya muji wenye kuta wa waadui.


Bwana, Yawe, Mungu wako, anayewatetea watu wake, anasema hivi: Nimekuondolea kikombe cha kuyumbisha, hautakunywa tena kikombe cha kasirani yangu.


Basi, malaika wa Yawe aliingia ndani ya kambi ya Waasuria na kuwaua watu elfu mia moja makumi nane na watano. Kesho yake, wakati watu walipoamuka, waliona yale maiti yote.


Hapo Waasuria watauawa kwa upanga, lakini si upanga wa watu; wataangamizwa kwa upanga ambao ni zaidi ya ule wa wanadamu. Waasuria watakimbia na vijana wao watatumikishwa kazi za kitumwa.


Enyi watu wa Sayuni, enyi watu wa Yerusalema, hakika ninyi hamutaomboleza tena. Kweli Mungu atawahurumia; mara tu atakaposikia kilio chenu atawaitikia.


Wakati wa magaribi yanaleta hofu kubwa, lakini mbele ya asubui yametoweka! Ndilo litakalowapata wale wanaotukamata na kutunyanganya mali yetu.


Utaingia ndani ya inchi ya Yuda kwa nguvu na kufurika na kupanda mpaka kwenye shingo. Utaenea juu ya inchi yako yote, ee Emanueli!


Wakati ule, Bwana atalipa wembe kutoka ngambo ya muto Furati, ni kusema mufalme wa Asuria. Atawanyoa vichwa vyenu, miili yenu na ndevu zenu vilevile.


Siku moja wakati Saniharibu alipokuwa akiabudu katika nyumba ya Nisiroki mungu wake, wana wake wawili, Adarameleki na Sarezeri walimwua kwa upanga, halafu wakakimbilia katika inchi ya Ararati. Halafu mwana wake Esari-Hadoni akatawala kwa pahali pake.


Basi, malaika wa Yawe aliingia ndani ya kambi ya Waasuria na kuwaua watu elfu mia moja makumi nane na watano. Kesho yake, wakati watu walipoamuka, waliona yale maiti yote.


“Usiku ule, nitapita katika inchi ya Misri na kuwaua wazaliwa wa kwanza wa Misri, watu na nyama. Nitaiazibu miungu yote ya Misri. Mimi ni Yawe.


Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe wa majeshi, atawaletea waaskari wao wanene ugonjwa wa kuwakondesha, na utukufu wao utateketezwa kama kwa moto.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite