Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Nahumu 1:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Watateketezwa kama kichaka cha miiba, wao wanaoikalia kulewa. Watateketezwa kama vile majani yenye kukauka.

Gade chapit la Kopi




Nahumu 1:10
19 Referans Kwoze  

Mutu muzuri zaidi kati yao ni kama michongoma, naye mwenye usawa zaidi ni hatari kama upango wa miiba. Siku iliyongojewa ya azabu yao imefika. Na sasa mahangaiko yamewapata.


Ninawe, nawe vilevile utalewa; utamukimbia adui na kujaribu kujificha.


Kwa kasirani ya Yawe wa majeshi inchi imechomwa moto, na watu ni kama kuni za kuuwasha. Hakuna mutu anayemuhurumia ndugu yake;


Kwa hiyo, kama vile moto unavyoteketeza nyasi, kama vile majani yanavyotoweka ndani ya moto, ndivyo mizizi yao itakavyooza, na maua yao yatakavyopeperushwa juu kama mavumbi. Maana wameacha sheria ya Yawe wa majeshi, wamezarau neno la yule Mutakatifu wa Israeli.


Nitawalewesha wakubwa na wenye hekima wake, watawala wake, maliwali na waaskari wake; watalala usingizi wa milele wala hawataweza tena kuamuka. –Ni ujumbe wa mufalme, jina lake Yawe wa majeshi!


Wakiwa na hamu kubwa nitawatayarishia karamu: nitawalewesha mpaka wapepesuke; nao watalala usingizi wa siku zote na hawataamuka tena. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Silikasirikii tena shamba hili; kama miiba na michongoma ingelilishambulia, mimi ningepambana nayo na kuichoma kwa moto.


Mungu asimame sasa, na waadui zake watawanyike! Wanaomuchukia wakimbie mbali naye!


Abusaloma akawaambia watumishi wake: “Mumwangalie Amunoni atakapokuwa amekunywa divai na kufurahi. Nitakapowaambia: ‘Mumupige Amunoni’, mumwue. Hiyo ni amri yangu kwenu. Mujipe moyo na mukuwe hodari.”


Abigaili aliporudi kwake, alimukuta Nabali akifanya karamu kubwa katika nyumba yake kama ya kifalme. Nabali alikuwa akifurahi sana ndani ya moyo maana alikuwa amelewa sana. Kwa hiyo hakumwambia neno lolote mpaka asubui.


Yalinizunguka, mengi kama nyuki, lakini yakateketea kama kichaka ndani ya moto; kwa jina la Yawe niliyaangamiza!


Wao ni kama majani yenye kukauka: moto utayateketeza! Hawawezi hata kujiokoa wenyewe mbali na ukali wa moto huo. Moto huo si wa kujipatia joto, huo si moto wa kuota!


Wao wanaambiana hivi: Mukuje, tuende kutafuta divai; mukuje tukunywe tushibe kinywaji kikali! Kesho itakuwa kama leo, tena itakuwa sikukuu kubwa zaidi.


Basi, watu wote wakatawanyika kila pahali katika inchi ya Misri wakitafuta nyasi za kutengeneza matofali.


Kwa wingi wa ukubwa wako unawaangamiza wapinzani wako; unawapulizia kasirani yako nayo inawateketeza kama maganda.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite