Lakini kutokea siku hiyo, Yoshua akawafanya hao kuwa wakata - kuni na wachota - maji kwa ajili ya Waisraeli wote na kwa ajili ya mazabahu ya Yawe, popote pale Yawe alipochagua mpaka hivi leo.
“Kisha mufalme atawaambia wale wanaokuwa kwa upande wake wa kushoto: ‘Muondoke hapa karibu nami, ninyi muliolaaniwa! Muende katika moto usiozimika hata milele, uliotayarishwa kwa ajili ya Shetani na wamalaika wake!
Kisha Yawe akamwambia nyoka: “Kwa sababu umefanya hivyo, umelaaniwa kuliko nyama wote wa kufugwa, na kuliko nyama wote wa pori. Utatambaa kwa tumbo lako na kula mavumbi siku zote za maisha yako.