Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 9:22 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

22 Hamu, baba ya Kanana, akaona uchi wa baba yake, akatoka inje na kuwaambia wandugu zake wawili.

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 9:22
17 Referans Kwoze  

Kama mutu akimuchekelea baba yake na kuzarau utii kwa mama yake, macho yake yataondolewa na kibombobombo wa pori na kuliwa na tai.


Wandugu zangu, kama mutu akipatikana na kosa fulani, ninyi munaoongozwa na Roho wa Mungu mumwonye mutu yule kwa roho ya upole. Na kila mumoja wenu ajiangalie mwenyewe, kusudi asijaribiwe vilevile.


Upendo haufurahii ubaya, lakini unafurahia ukweli.


“Kama ndugu yako akikukosea, umwendee kwa kumwonyesha kosa lake, mukiwa ninyi wawili peke yenu. Na kama akikusikia, unarudiliana na ndugu yako.


Wapate haya na kufezeheka wanaotaka kuniua! Warudi nyuma na kufezeheka wanaonitakia hasara!


Wote wanaokusudia kuniangamiza, wafezeheke pamoja! Hao wanaotamani niumie, warudi nyuma na kuzarauliwa!


Wana wa Hamu walikuwa Kushi, Misiraimu, Puti na Kanana.


Utengeneze ugomvi na mwenzako peke yake, na kila mumoja wenu asitoe siri ya mwenzake;


Wana wa Hamu walikuwa baba za watu walioishi katika inchi ya Etiopia, Misri, Puti na Kanana. Wana wa Etiopia walikuwa: Seba, Havila, Sabuta, Rama na Sabuteka. Etiopia alizaa vilevile Nimurodi, aliyekuwa mutu shujaa wa kwanza katika dunia. Wana wa Rama walikuwa: Seba na Dedani.


akasema: “Kanana alaaniwe! Atakuwa mutumwa wa watumwa kwa wandugu zake.”


Lakini Semu na Yafeti wakatwaa nguo, wakaiweka juu ya mabega yao, wakakwenda kinyumenyume na kufunika uchi wa baba yao. Waliangalia pembeni, wala hawakuuona uchi wa baba yao.


Ole wako unayewalewesha jirani zako, na kutia sumu katika divai yao kusudi upate kuwaona wakiikaa uchi.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite