Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 9:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 nitakumbuka agano langu nanyi na viumbe vyote vyenye uzima. Maji hayatageuka hata kidogo kuwa mafuriko ya kuangamiza viumbe vyote vyenye uzima.

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 9:15
14 Referans Kwoze  

Basi, mujue kwamba Yawe, Mungu wenu, ndiye Mungu. Yeye ni Mungu mwaminifu, anayeshika agano lake na kutenda mema kwa vizazi vingi vya wale wanaomupenda na kushika amri zake.


Lakini mimi nitalikumbuka agano langu nililoagana nawe katika siku za ujana wako. Nitafanya nawe agano la milele.


kwa ajili yao alilikumbuka agano lake, akawahurumia kwa wingi wa wema wake.


akasema: “Ee Yawe, Mungu wa Israeli, hakuna Mungu mwingine kama wewe, juu mbinguni, au chini katika dunia. Wewe unashika agano lako na kutenda wema kwa watumishi wako wanaoishi wakikutii kwa moyo wao wote.


Mawe hayo mawili yatawekwa juu ya mikaba ya kizibao kama vile ukumbusho wa makabila kumi na mawili ya Israeli. Hivyo Haruni atavaa majina hayo juu ya mabega yake mbele yangu mimi Yawe kama vile ukumbusho.


Aliahidi kuwasikilia babu zetu huruma; na kukumbuka agano lake takatifu,


Usitutupe, kwa ajili ya heshima ya jina lako; usikizarau kiti chako cha kifalme chenye utukufu. Ukumbuke agano ulilofanya nasi, wala usilivunje.


Kwa hiyo, ee Mungu wetu, Mungu mukubwa, mwenye nguvu na wa kutisha, wewe unashika agano lako na kutenda wema. Mateso yaliyotupata, sisi, wafalme wetu, wakubwa wetu, makuhani wetu, manabii wetu, babu zetu na watu wako wote tangu wakati wa wafalme wa Asuria mpaka leo, usiyaone kuwa ni madogo.


Harufu nzuri ya sadaka hiyo ikamupendeza Yawe, naye akasema ndani ya moyo wake: “Sitailaani tena inchi hata kidogo kwa sababu ya mwanadamu. Ninajua kwamba mawazo yake ni maovu tangu utoto wake. Wala sitaangamiza tena viumbe vyote kama vile nilivyofanya.


Ninasimamisha agano langu nanyi, kwamba hakutatokea tena mafuriko ya maji kwa kuangamiza inchi nzima au viumbe vyote vyenye uzima.”


Kila mara nitakapofunika dunia kwa mawingu, na huo upinde wa mvua utakapoonekana katika mawingu,


na viumbe vyote vyenye uzima, ndege, nyama wa kufugwa na wa pori, wote waliotoka katika chombo pamoja nanyi.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite