Mwanzo 8:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
1 Kisha Mungu akamukumbuka Noa na nyama wote wa pori na wa kufugwa waliokuwa pamoja naye ndani ya chombo. Basi, Mungu akavumisha upepo juu ya inchi, maji yakaanza kupunguka.
Mungu alipoangamiza miji katika bonde ambamo Loti alikuwa anakaa, alimukumbuka Abrahamu kwa kumutosha Loti katika miji hiyo, kusudi Loti asiangamizwe pamoja nayo.
Kesho yake asubui, Elekana na jamaa yake waliamuka asubui mapema, na kisha kumwabudu Yawe, walirudi kwao Rama. Elekana akalala na muke wake Hana na Yawe akamukumbuka.
Musa akanyoosha mukono wake juu ya bahari, naye Yawe akasukuma bahari nyuma kwa upepo mukali toka upande wa mashariki. Upepo ule ulivuma usiku kucha, ukagawanya bahari sehemu mbili na katikati kukatokea inchi kavu.
Ee Yawe, nimesikia juu ya utukufu wako, juu ya matendo yako, nami ninaogopa. Uyafanye tena mambo yale wakati wetu; uyafanye yajulikane wakati huu wetu. Unapokasirika tafazali ukumbuke huruma yako!
Ee Yawe, usisahau mambo Waedomu waliyotenda, siku ile Yerusalema iliponyanganywa; kumbuka maneno haya waliyosema: “Mubomoe Yerusalema! Muongoe hata na misingi yake!”
Nikaagiza matoleo ya kuni kufanyika katika wakati unaopaswa na malimbuko wakati wake. Ee Mungu wangu, unikumbuke kwa ajili ya haya yote na unijalie mema.
Nikaagiza Walawi kujitakasa na kwenda kulinda milango kwa kutakasa siku ya Sabato. Ee, Mungu wangu, unikumbuke hata na kwa hili vilevile unihurumie kutokana na rehema zako kubwa.
Na ule muji mukubwa ukagawanyika katika sehemu tatu, na miji ya mataifa yote ikabomoka. Mungu hakusahau muji mukubwa Babeli, akaukunywesha kikombe kinachokuwa na divai ya kasirani yake kali.
Basi, haifai kwangu kuuhurumia Ninawe, ule muji mukubwa wenye watu elfu mia moja na makumi mbili, wasioweza kutambua linalokuwa jema na baya; na nyama wengi wasiokuwa na hesabu?
Wakati wa vita katika inchi yenu juu ya waadui wanaowashambulia, mutatoa kitambulisho cha vita kwa kupiga baragumu hizi kusudi Yawe, Mungu wenu apate kuwakumbuka na kuwaokoa na waadui zenu.
Watapitia katika bahari ya mateso, nami nitayapiga mawimbi yake, na vilindi vya maji ya muto Nili vitakauka. Kiburi cha Asuria kitavunjwa na nguvu za Misri zitatoweka.