Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 7:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

23 Mungu akaangamiza kila kiumbe kilichokuwa na pumzi ya uzima katika dunia: wanadamu, nyama, viumbe vinavyotambaa na ndege wa anga. Vyote viliangamizwa katika dunia. Noa tu ndiye aliyebaki na wale waliokuwa pamoja naye ndani ya chombo.

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 7:23
21 Referans Kwoze  

Mungu hakuhurumia dunia ya zamani, lakini alimulinda Noa, muhubiri wa haki, pamoja na watu wengine saba alipoleta mafuriko ya maji juu ya dunia ile ya waovu.


Roho zile ni za watu walioasi Mungu zamani za kale alipowavumilia katika siku Noa alipotengeneza chombo kikubwa. Ni watu wanane tu ndio waliingia ndani ya chombo na kuokolewa katika maji.


Kwa njia ya imani, Noa alionywa na Mungu juu ya mambo yatakayotokea, yale aliyokuwa hajayaona bado. Yeye alimutii Mungu na kujenga chombo kwa kujiokoa yeye mwenyewe pamoja na jamaa yake. Kutokana na hayo yote akahukumu dunia na kupokea haki inayopatikana kwa njia ya imani.


Vilevile kufuatana na ile, dunia ya zamani iliangamizwa kwa mafuriko ya maji.


Halafu hawa watakwenda kwenye nafasi watakapoazibiwa kwa milele, lakini wenye haki wataingia kwenye uzima wa milele.”


Basi, ni kusema kwamba Bwana anajua namna ya kuwaokoa wenye kumwogopa katika majaribu. Lakini anangojea kuwaazibu watu wabaya kwa Siku ile ya hukumu.


Utajiri haufai kitu siku ya kasirani, lakini haki inaokoa kutoka kifo.


Ukikaa chini ya ulinzi wa Mungu Mukubwa, ukiishi chini ya kivuli cha Mungu Mwenye Nguvu,


Atakuokoa mara sita toka katika magumu; hata mara saba hasara haitakugusa.


Kama watu elfu wakianguka pembeni yako, hata elfu kumi karibu yako, hasara haitakupata.


Nitaleta mafuriko ya maji kwa kuangamiza viumbe vyote vyenye uzima katika dunia. Kila kiumbe chenye uzima katika dunia kitakufa.


Basi, Noa akatoka katika chombo pamoja na wana wake na muke wake pamoja na wake za wana wake.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite