Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 7:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Viumbe vyote vyenye uzima katika inchi vikakufa: ndege, nyama wa kufugwa, nyama wa pori, nyama wadogowadogo katika inchi kavu na wanadamu wote;

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 7:21
20 Referans Kwoze  

Mungu akamwambia Noa: “Nimeamua kuwaangamiza wanadamu wote kwa sababu wamejaza dunia mateso makali. Hakika, nitawaangamiza kabisa pamoja na dunia!


Nyuma ya siku saba, nitanyesha mvua juu ya inchi siku makumi ine muchana na usiku, na kila kiumbe chenye uzima nilichokiumba katika dunia nitakiangamiza.”


Nitaleta mafuriko ya maji kwa kuangamiza viumbe vyote vyenye uzima katika dunia. Kila kiumbe chenye uzima katika dunia kitakufa.


Kwa maana viumbe vyote vimewekwa chini ya utawala wa mambo ya ovyo, si kwa mapenzi yao, lakini kwa sababu ya yule aliyewatia katika hali hiyo. Lakini kungali tumaini hili:


Mungu hakuhurumia dunia ya zamani, lakini alimulinda Noa, muhubiri wa haki, pamoja na watu wengine saba alipoleta mafuriko ya maji juu ya dunia ile ya waovu.


Kwa maana tunajua kwamba mpaka sasa viumbe vyote vinaugua kwa uchungu kama mwanamuke anayesikia maumivu ya kuzaa.


Siku zile watu walikuwa wakikula na kunywa, wakioa na kuolewa mpaka ilipotimia siku ile Noa alipoingia ndani ya chombo. Halafu mvua kubwa ikanyesha na kuwaangamiza wote.


Nao hawakutambua kitu mpaka mvua kubwa sana ilipotokea, na kuwaua wote. Na ni hivi itakavyokuwa wakati Mwana wa Mutu atakaporudi.


wanadamu, nyama, ndege na samaki. Vyote nitaviangamiza. Waovu nitawaangamiza kabisa; wanadamu nitawateketeza kabisa katika dunia.


Kama vile moto unavyoteketeza, Jeshi hilo linaharibu kila kitu mbele yake na kuacha nyuma kila kitu kinateketezwa; mbele ya kupita kwao, inchi ni kama bustani ya Edeni, lakini wakisha kupita, ni jangwa tupu. Hakuna kinachoweza kuponyoka!


Kwa hiyo, inchi yote inakauka, wakaaji wake wote wanaangamia pamoja na nyama na ndege; hata samaki wanaangamizwa.


Dunia inavunjikavunjika, inapasuka na kutikiswatikiswa.


Kwa sababu hiyo laana inaiteketeza dunia, wakaaji wake wanateseka kwa ajili ya makosa yao. Wakaaji wa dunia wamepunguka, ni watu wachache tu waliobaki.


Mungu akafanya aina zote za nyama wa pori, nyama wa kufugwa, na viumbe vinavyotambaa. Mungu akaona kwamba ni vizuri.


viumbe vyote vingeangamia kabisa, naye mwanadamu angerudi katika mavumbi.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite