Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 6:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Hizi ndizo habari za Noa na uzao wake. Noa alikuwa mwenye haki na mukamilifu kati ya watu wa wakati ule. Aliishi katika ushirika na Mungu.

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 6:9
34 Referans Kwoze  

Wote wawili walikuwa wenye haki mbele ya Mungu, walishika kwa ukamilifu amri na maagizo yote ya Bwana.


Kwa njia ya imani, Noa alionywa na Mungu juu ya mambo yatakayotokea, yale aliyokuwa hajayaona bado. Yeye alimutii Mungu na kujenga chombo kwa kujiokoa yeye mwenyewe pamoja na jamaa yake. Kutokana na hayo yote akahukumu dunia na kupokea haki inayopatikana kwa njia ya imani.


Mungu hakuhurumia dunia ya zamani, lakini alimulinda Noa, muhubiri wa haki, pamoja na watu wengine saba alipoleta mafuriko ya maji juu ya dunia ile ya waovu.


Yawe akamwambia Noa: “Ingia ndani ya chombo wewe pamoja na jamaa yako yote, kwa maana, kati ya watu wote wa kizazi hiki, nimekuona wewe peke yako kuwa mutu wa haki mbele yangu.


Alikuwa akishirikiana na Mungu, akatoweka, kwa maana Mungu alimupeleka.


Na zaidi ya hii ni wazi kwamba hakuna mutu anayehesabiwa haki mbele ya Mungu kwa njia ya Sheria. Kwa maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Mwenye haki ataishi kwa njia ya imani.”


Wakati Abramu alipokuwa na umri wa miaka makumi tisa na tisa, Yawe akamutokea, akamwambia: “Mimi ni Mungu Mwenye Uwezo. Uendelee mbele yangu na kuwa mukamilifu.


Enoki alikuwa anashirikiana na Mungu. Kisha kuzaa Metusela, Enoki aliishi miaka mia tatu, na kupata wana wengine na wabinti.


Hata kama Noa, Danieli na Yobu wangalikuwa ndani ya inchi ile, wangeyaokoa tu maisha yao wenyewe kwa ajili ya haki yao. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–


Kulikuwa mutu mumoja katika inchi ya Usi, aliyeitwa Yobu. Mutu yule alikuwa mukamilifu, wa usawa, mwenye kumwogopa Mungu na mwenye kuepukana na uovu.


Hivi ndivyo mbingu na dunia zilivyoumbwa. Siku ile Yawe Mungu alipoumba mbingu na dunia,


Nanyi vilevile, kama mawe yenye uzima mutumiwe kwa kujenga hekalu la kiroho. Na mule mutafanya kazi takatifu ya ukuhani kwa kutoa sadaka za kiroho zinazomupendeza Mungu kwa njia ya Yesu Kristo.


Hakika, hakuna mutu wa haki katika dunia anayetenda vizuri siku zote bila kutenda zambi.


Nao wakamujibu: “Tumetumwa hapa na Kornelio, mukubwa wa waaskari. Yeye ni mutu wa haki na mwenye kumutii Mungu, naye anasifiwa na Wayuda wote. Malaika mutakatifu amemutokea na kumwagiza akuite ufike kwake kusudi asikie maneno utakayomwambia.”


Na hata kama Noa, Daneli na Yobu wangelikuwa ndani ya inchi ile, kama vile ninavyoishi, –ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe– hawangeweza kuwaokoa hata mwana au binti. Wangeyaokoa tu maisha yao wenyewe kwa ajili ya haki yao.


Yawe akamwambia Shetani: “Umemwona vizuri mutumishi wangu Yobu? Katika dunia hakuna mwingine anayekuwa kama yeye. Yeye ni mutu mukamilifu, wa usawa, mwenye kumwogopa Mungu na mwenye kuepukana na uovu.”


Kwa maana Habari Njema inaonyesha namna Mungu anavyowahesabia watu haki mbele yake. Jambo hilo haliwezekani isipokuwa kwa njia ya kuamini tu. Ni sawa vile inavyoandikwa katika Maandiko Matakatifu yanayosema: “Mwenye haki ataishi kwa njia ya imani.”


Kulikuwa mutu mumoja muzaliwa wa Arimatea, katika jimbo la Yuda, jina lake lilikuwa Yosefu. Mutu huyu alikuwa mwema na mwenye haki, naye alikuwa akitazamia Ufalme wa Mungu. Yeye alikuwa mumoja wa washauri wa Baraza Kubwa, lakini hakukubali shauri na matendo ya wenzake.


Wakati ule katika Yerusalema kulikuwa mutu mumoja aliyeitwa Simeoni. Mutu huyo alikuwa mwenye haki na mwenye kuogopa Mungu. Alikuwa akitazamia kwa hamu ukombozi wa taifa la Israeli. Roho Mutakatifu alikuwa pamoja naye;


Andika: Uwaangalie wenye kiburi, hao wataangamia; lakini wenye haki wataishi kwa kumwamini Mungu.


Njia ya wenye haki ni kama mwangaza wa asubui mapema, ambao unaangaza zaidi na zaidi hata muchana kamili.


Muangalie mutu mukamilifu, mutu wa usawa; mutu anayependa amani anajaliwa wazao.


Lakini hata hivyo pahali pa kutambikia miungu mingine katika Israeli hapakuharibiwa; lakini yeye alikuwa na moyo mwaminifu maisha yake yote.


Kisha Israeli akamubariki Yosefu, akisema: “Mungu ambaye babu zangu Abrahamu na Isaka walimutii katika maisha yao, Mungu ambaye ameniongoza katika maisha yangu mpaka leo,


Nilikuwa mutu wa kumwomba Mungu na kupata jibu lake. Sasa, watu wananichekelea. Wanachekelea mutu mukamilifu, mwenye haki.


Solomono akamwambia: “Ulimwonyesha wema mwingi mutumishi wako Daudi, baba yangu, kwa sababu alikutumikia kwa uaminifu, kwa haki na kwa moyo wa usawa; na umedumisha mema yako kwa kumupa mwana anayeikaa sasa kwenye kiti chake cha kifalme.


Alitenda kwa usawa mbele ya Yawe ingawa hakutenda kwa moyo mukamilifu.


Nyuma ya mafuriko ya maji, Semu, Hamu na Yafeti, wana wa Noa, walipata watoto wanaume na wanawake. Hawa ndio wazao wao:


Hiki ndicho kitabu cha uzao wa Adamu. Wakati Mungu alipowaumba wanadamu, aliwaumba kwa mufano wake.


Noa alikuwa na wana watatu: Semu, Hamu na Yafeti.


Mukuwe wakamilifu mbele ya Yawe, Mungu wenu.


Mbele yake nilikuwa mukamilifu, nimejikinga nisikuwe na kosa.


Yawe anawaokoa watu wa haki, na kuwalinda wakati wa taabu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite