Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 6:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Hivyo akasema: “Nitamuharibu kabisa katika dunia mwanadamu niliyemwumba, pamoja na nyama wa pori, viumbe vinavyotambaa na ndege wa anga. Ninasikitika kwamba niliwaumba katika dunia.”

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 6:7
21 Referans Kwoze  

wanadamu, nyama, ndege na samaki. Vyote nitaviangamiza. Waovu nitawaangamiza kabisa; wanadamu nitawateketeza kabisa katika dunia.


Lakini waovu wataangamia, waadui za Yawe watanyauka kama maua katika jangwa; kweli watatoweka kama moshi.


Yawe ameumba kila kitu kwa kusudi lake, hata waovu kwa ajili ya siku ya maangamizi.


Kumwogopa Yawe kunarefusha maisha, lakini miaka ya waovu itakuwa mifupi.


Kwa hiyo, inchi yote inakauka, wakaaji wake wote wanaangamia pamoja na nyama na ndege; hata samaki wanaangamizwa.


Yawe akasikitika sana kwa kumwumba mwanadamu katika dunia. Yawe akahuzunika sana ndani ya moyo wake.


Nyuma ya siku saba, nitanyesha mvua juu ya inchi siku makumi ine muchana na usiku, na kila kiumbe chenye uzima nilichokiumba katika dunia nitakiangamiza.”


Viumbe vyote vyenye uzima katika inchi vikakufa: ndege, nyama wa kufugwa, nyama wa pori, nyama wadogowadogo katika inchi kavu na wanadamu wote;


Harufu nzuri ya sadaka hiyo ikamupendeza Yawe, naye akasema ndani ya moyo wake: “Sitailaani tena inchi hata kidogo kwa sababu ya mwanadamu. Ninajua kwamba mawazo yake ni maovu tangu utoto wake. Wala sitaangamiza tena viumbe vyote kama vile nilivyofanya.


Kama vile Yawe alivyopendezwa kuwafanikisha na kuwafanya kuwa wengi, ni vile vile Yawe atapendezwa kuwaletea hasara na kuwaangamiza. Nanyi mutaondolewa katika inchi hiyo ambayo munakwenda kuirizi.


Yawe atamutenga kutoka kati ya makabila yote ya Israeli apatwe na hasara kufuatana na laana zote za agano zilizoandikwa katika kitabu hiki.


“Ninajuta kwamba nimemufanya Saulo kuwa mufalme. Yeye ameacha kunifuata mimi na hajatimiza amri zangu.” Samweli alikasirika, akamulilia Yawe usiku kucha.


Basi, Bwana wetu Yawe akabadilisha nia yake, akasema: Halitatukia!


Basi, Yawe akabadilisha nia yake, akasema: Hili vilevile halitatukia.


Nitateketeza kabisa viumbe vyote katika dunia:


Feza yao wala zahabu yao havitaweza kuwaokoa katika siku hiyo ya kasirani ya Yawe. Kwa moto wa wivu wake dunia yote itateketezwa. Kwa ukamilifu na kwa namna ya kuogopesha atawafanya wakaaji wote katika dunia watoweke.


Matawi ya miti yamekauka na kuvunjika; wanawake wanayaokota na kuyawasha moto. Watu hawa hawajaelewa kitu, kwa hiyo Mungu, Muumba wao, hatawahurumia, yeye aliyewafanya, hatawatendea mema.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite