Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 6:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 wana wa Mungu wakaona kwamba wale wabinti za watu ni wazuri, wakawatwaa wale waliowapendeza kuwa wake zao.

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 6:2
31 Referans Kwoze  

Kwa maana kila kitu kinachokuwa katika dunia, kama vile tamaa ya kimwili, tamaa ya macho, na majivuno ya maisha, hivi vyote havitoki kwa Baba, lakini vinatoka katika dunia.


Macho yao yanajaa uzinzi. Wao hawachoki kufanya zambi. Wanavuta watu wasiokamilika. Wanatawaliwa na tamaa za kupata mali. Watu hao wamelaaniwa!


Kwa hiyo, musiwaoeshe na wabinti zenu kwa watu hao, wala musiwaruhusu wana wenu kuwaoa wabinti zao. Pia, musishugulikie usalama au mafanikio yao, kusudi ninyi wenyewe mupate kuwa na nguvu, na mufaidie mema ya inchi hiyo na kuwaachia watoto wenu kama vile urizi milele.’


Siku moja, wakati wa magaribi, Daudi aliamuka toka katika kitanda, akaenda kwenye dari ya nyumba ya kifalme. Alipokuwa anatembea kule juu, alimwona mwanamuke mumoja akioga na mwanamuke yule alikuwa muzuri sana kwa umbo.


“Ninyi ni watoto wa Yawe, Mungu wenu; musijichanje wala kunyoa nywele upande wa mbele kwa ajili ya mutu aliyekufa.


Vijana wenu wakioa wabinti zao, na hao wabinti wanaoabudu miungu yao, watawashawishi vijana wenu kufuata miungu yao.


Rebeka akamwambia Isaka: “Sina raha kabisa katika maisha kwa sababu ya hawa wanawake Wahiti wa Esau. Ikiwa Yakobo ataoa mumoja wa wanawake hawa Wahiti, maisha yangu yana faida gani?”


nami nitakuapisha kwa jina la Yawe, Mungu wa mbingu na dunia, kwamba hautamwoea mwana wangu binti yeyote kati ya wabinti za Wakanana ninaoishi nao.


Seti naye akapata mutoto mwanaume, akamwita Enosi. Hapo ndipo watu walipoanza kumwomba Yawe kwa jina lake.


Basi, mwanamuke alipoona kwamba muti ule ni muzuri kwa chakula, unavutia macho, na kwamba unafaa kwa kupata hekima, akachuma tunda lake, akakula, akamupa mume wake aliyekuwa pamoja naye, naye vilevile akakula.


Nitakuwa Baba yenu nanyi mutakuwa wana na wabinti wangu. Ni mimi Bwana Mwenye Uwezo ninayesema.”


Mwanamuke aliyeolewa anafungwa na Sheria katika maisha yake na mume wake wakati mume wake angali muzima. Lakini kama mume wake akikufa, yeye ni huru kuolewa na yule anayetaka, lakini sherti ndoa ikuwe ya kikristo.


Mungu hakuwafanya ninyi wote wawili mukuwe mwili mumoja na roho moja? Alikusudia nini alipofanya hayo? Tuzae watoto wanaomupendeza Mungu. Kwa hiyo, muchunge uzima wenu na kuhakikisha kwamba hakuna hata mumoja wenu anayekosa uaminifu kwa muke wake.


Watu wa Yuda wamekosa uaminifu kwa Mungu na kutenda machukizo katika Israeli na katika Yerusalema. Wamechafua hekalu la Yawe analolipenda. Tena wameoa wanawake wanaoabudu miungu ya kigeni.


Maana wewe ndiwe Baba yetu; Abrahamu, babu yetu, hatujali, naye Israeli hatutambui; lakini wewe, ee Yawe, ni Baba yetu. Wewe umeitwa tangu zamani: Mukombozi wetu.


Nimejizuiza kabisa mimi mwenyewe, macho yangu yasimwangalie binti kwa tamaa.


Wakati watu walipoanza kuongezeka katika dunia na kuzaa wabinti,


Kwa hiyo, Yawe akasema: “Roho yangu haitakaa ndani ya wanadamu milele, maana yeye ni wa kufa tu. Basi, hataishi zaidi ya miaka mia moja na makumi mbili.”


Alipokaribia Misri, Abramu akamwambia Sarai muke wake: “Ninajua kwamba wewe ni mwanamuke muzuri na wa kuvutia.


Wanawake hao walifanya maisha ya Isaka na Rebeka kuwa machungu.


Basi, ikatukia siku moja wamalaika wa Mungu walikwenda kukutana mbele ya Yawe. Shetani akakuja kuwa pamoja nao.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite