Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 49:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Atafunga punda wake katika muzabibu na mwana-punda wake kwenye muzabibu bora. Atafua nguo zake katika divai, na kanzu zake katika divai nyekundu.

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 49:11
15 Referans Kwoze  

Nami nikamujibu: “Bwana wangu wewe ndiwe unayejua.” Naye akaniambia: “Hawa ndio wanaotoka katika mateso makubwa. Wamesafisha kanzu zao na kuzifanya kuwa nyeupe katika damu ya Mwana-Kondoo.


Hivi mutakula nyama za miili ya wafalme, za majemadari, za watu wenye uwezo, nyama za farasi pamoja na za watu wanaopanda juu yao na nyama za watu wote wanaokuwa huru na za watumwa, wakubwa kama vile wadogo.”


Kila mutu atakaa kwa amani chini ya miti ya tini na mizabibu yake, bila kutishwa na mutu yeyote. –Maneno haya yanatoka katika kinywa cha Yawe wa majeshi.


Watu wa Yuda na wa Israeli walikuwa wengi kama muchanga wa bahari, nao walikuwa wakikula, wakikunywa, na kufurahi.


mpaka nitakapokuja na kuwapeleka katika inchi kama hii yenu, inchi yenye ngano na divai, inchi yenye mukate na mashamba ya mizabibu, inchi yenye mizeituni na asali, kusudi mupate kuishi, nanyi hamutakufa. Musimusikilize Hezekia anapowadanganya akisema: Yawe atatuokoa.


Zile zabibu zikakamuliwa mbali na muji, damu ikatiririka toka ndani ya kile kikamulio mpaka ikafika kwenye umbali wa kilometre yapata mia tatu. Nao urefu kwenda chini wa ile damu ulikuwa yapata metre moja na nusu.


Macho yake ni mekundu kwa divai, meno yake ni meupe kwa maziwa.


Yawe, Mungu wenu, anawaleta kwenye inchi nzuri, inchi yenye vijito na chemichemi, na maji yanayobubujika kutoka bonde na milima;


inchi yenye ngano na shayiri, mizabibu, mitini, mikomamanga, mizeituni na asali.


Aliwapa siagi na maziwa ya mifugo, mafuta ya wana-kondoo na kondoo dume, makundi ya mifugo ya Basani na mbuzi. Aliwapa ngano nzuri kabisa na divai mupya wakakunywa.


Siku zinakuja ambapo wakati wa kuvuna utafuata mbio wakati wa kulima, wakati wa kukamua zabibu utafuata mbio wakati wa kupanda mizabibu. –Ni ujumbe wa Yawe.– Milima itabubujika divai mupya, navyo vilima vitatiririka divai.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite