Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 47:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Kisha, Yosefu akamuleta baba yake Yakobo kumwamukia mufalme. Naye Yakobo akamupa mufalme baraka zake.

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 47:7
18 Referans Kwoze  

Kisha Yakobo akamubariki mufalme, akaondoka.


Muwaheshimu watu wote. Muwapende wandugu zenu waamini. Mumwogope Mungu, mumuheshimu mufalme.


Halafu akatwaa mukate, akaubariki, kisha akaumega na kuwapa akisema: “Huu ni mwili wangu [unaotolewa kwa ajili yenu. Mufanye hivi kwa kunikumbuka.”


Walipokuwa wakikula, Yesu akatwaa mukate, akaubariki, kisha akaumega na kuwapa wanafunzi wake, akisema: “Mutwae na mukule, huu ni mwili wangu.”


Elisha akamwambia Gehazi: “Ujitayarishe kusafiri, twaa fimbo yangu, na uende mara moja. Usisimame katika njia kwa kumusalimia mutu yeyote, na mutu yeyote akikusalimia katika njia, usipoteze wakati kwa kumurudishia salamu. Kwenda moja kwa moja mpaka katika nyumba na kuweka fimbo yangu juu ya uso wa mutoto.”


Zaidi ya hayo, watumishi wa mufalme walikuja kumupa pole bwana wetu mufalme Daudi wakisema: ‘Mungu wako alifanye jina la Solomono kuwa lenye sifa kuliko lako; tena akitukuze kiti chake cha kifalme kuliko kiti chako.’ Halafu mufalme akainama juu ya kitanda


Mufalme akamwambia: “Kimuhamu atakwenda nami, na nitamutendea lolote unaloona ni zuri. Na lolote utakalotaka nikutendee, nitakutendea.”


Yoabu alianguka uso mpaka chini, na kumutakia mufalme baraka, akasema: “Leo, mimi mutumishi wako, bwana wangu mufalme, ninajua kwamba nimepata kukubaliwa mbele yako, kwa kulikubali shauri langu.”


alimutuma mwana wake Yoramu kwa mufalme Daudi kwa kumupelekea salamu na shukrani kwa sababu alikuwa amepigana na Hadadezeri na kumushinda. Maana Hadadezeri alipigana na Toi mara nyingi. Yoramu alimupelekea Daudi zawadi za vyombo vya feza, zahabu na shaba.


Eli aliwabariki Elekana na muke wake, akisema: “Yawe akupe wewe Elekana watoto wengine kwa mwanamuke huyu kusudi wakamate nafasi ya yule uliyemupa Yawe.” Kisha wao walirudi kwao.


Halafu Yoshua akamubariki Kalebu mwana wa Yefune na kumupa muji wa Hebroni kuwa sehemu yake.


Mutwae makundi yenu ya kondoo na ngombe, muondoke. Muniombee na mimi baraka.”


Yakobo akaondoka akakwenda Mamure kwa baba yake Isaka, kule Kiriati-Arba ni kusema Hebroni, pahali ambapo Abrahamu na Isaka walikaa kama wageni.


Mufalme akamwuliza Yakobo: “Umri wako ni miaka mingapi?”


Basi, Yoshua akawabariki na kuwaruhusu waende zao akawaambia:


Katika siku ya nane, Solomono aliwaaga watu; nao wakamutakia mufalme baraka, wakaenda kwao wakishangilia na kufurahi kwa sababu ya wema ambao Yawe aliuonyesha kwa Daudi, mutumishi wake, na kwa watu wake Waisraeli.


akamubariki Abramu akisema: “Abramu abarikiwe na Mungu Mukubwa, Muumba wa mbingu na dunia!


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite