Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 47:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Yosefu akakuwa anawapatia baba yake, wandugu zake na jamaa yote ya baba yake chakula kulingana na hesabu ya watu waliowategemea.

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 47:12
16 Referans Kwoze  

Utakapokuwa Goseni, mimi nitakutunza wewe na jamaa yako pamoja na nyama wako kusudi musikufe na njaa, maana kungali miaka mitano zaidi ya njaa.’ ”


Kama mutu asipotunza wandugu zake na hasa zaidi watu wa jamaa yake mwenyewe, huyu amekana imani yake naye ni mubaya kuliko mupagani.


Lakini kama mujane akiwa na watoto au wajukuu, inafaa wajifunze kwanza kutimiza mapaswa yao ya kidini kwa ajili ya jamaa zao wenyewe na kuwarudishia wazazi na babu zao mema waliyowatendea, kwa maana jambo hilo linamupendeza Mungu.


Mazoezi ya mwili yana mafaa kidogo, lakini kushikamana na ibada kuna mafaa katika mambo yote, kwa maana kunatupatia ahadi ya kuishi kwa wakati huu wa sasa na kwa wakati utakaokuja.


ijapokuwa sisi ni mitume wa Kristo, tungeweza kudai mambo fulani kwenu. Lakini sisi tulionyesha upole kati yenu kama vile mama anavyosumbuka kwa ajili ya watoto wake.


Yeye atakurudishia uzima wako na atakutunza katika uzee wako. Mukwe wako ni wa lazima zaidi kwako kuliko watoto wa kiume saba, maana anakupenda na amekuzalia mujukuu huyu!”


Uwaheshimu baba yako na mama yako, kusudi uishi maisha marefu katika inchi ninayokupatia mimi Yawe, Mungu wako.


Wakati wa mavuno, sehemu moja ya tano mutamupa mufalme. Sehemu ine zitakazobaki zitakuwa mbegu na chakula kwa ajili yenu na jamaa zenu na watoto wenu.”


na Yosefu akawafanya watu kuwa watumwa, kutoka pembe moja mpaka pembe ingine ya inchi ya Misri.


Basi, Yosefu akakwenda kwa mufalme wa Misri, akamwambia: “Baba yangu na wandugu zangu pamoja na kondoo, ngombe na mali yao yote, wamefika kutoka inchi ya Kanana. Sasa wako katika eneo la Goseni.”


Basi, musiogope. Mimi nitawapa chakula pamoja na watoto wenu.” Basi akawafariji na kusema nao vizuri.


Mungu alinileta huku niwatangulie ninyi, kwa kuokoa maisha yenu mubaki wazima katika inchi na kuwakomboa kwa ukombozi mukubwa.


Utakaa karibu nami katika eneo la Goseni: wewe, wana wako na wajukuu wako, nyama wako wa kufugwa na mali yako yote.


Watu wote na jamaa yake, wadogo kwa wakubwa watajitegemeza kwake kama chungu na vikombe vilivyotundikwa kwenye musumari.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite