Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 42:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Basi, wana wa Israeli wakafika Misri wakiwa kati ya wanunuzi wengine, maana hata katika inchi ya Kanana kulikuwa njaa.

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 42:5
7 Referans Kwoze  

Halafu kukatokea njaa kubwa na mateso mengi katika inchi yote ya Misri na ya Kanana, nao babu zetu wakakuwa katika ukosefu wa chakula.


Zaidi ya hayo, watu toka kila pahali katika dunia walikuja Misri kwa Yosefu kununua ngano, maana njaa ilikuwa kali katika dunia yote.


Wakati ule, njaa ikatokea katika inchi. Njaa hiyo ilikuwa kali, hivyo Abramu akalazimika kwenda Misri kukaa kule kwa muda.


Kisha kukatokea njaa katika inchi ile, nyuma ya ile ya kwanza iliyokuwa kwa wakati wa Abrahamu. Isaka akakwenda Gerari kwa Abimeleki mufalme wa Wafilistini.


Na mumoja wao, aliyeitwa Agabo, akasimama, akatabiri kwa njia ya Roho Mutakatifu kwamba kutakuwa njaa kubwa katika dunia nzima. (Nayo ikatokea katika nyakati za utawala wa mufalme Klaudio wa Roma.)


Wakati mumoja katika siku za utawala wa Daudi kukatokea njaa kali katika inchi. Njaa hiyo ilidumu miaka mitatu yenye kufuatana. Daudi alimwomba Yawe shauri. Yawe akamwambia: “Saulo na jamaa yake wana makosa ya kumwanga damu kwa sababu aliwaua Wagibeoni.”


Ikaanza miaka saba ya njaa kama vile Yosefu alivyokuwa amesema pale mbele. Inchi zingine zote zikakuwa na njaa, lakini inchi yote ya Misri ilikuwa na chakula.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite