6 Yawe akamwambia Kaina: “Kwa nini umekasirika, na kwa nini uso wako umekunjamana?
Yawe anasema hivi: Mukuje basi, tukate shauri. Zambi zenu zikionekana kuwa nyekundu, zitakuwa nyeupe kama teluji; zikionekana kuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama sufu.
Kweli mahangaiko yanamwua mupumbafu, na wivu unamwangamiza mujinga.
Sina haki ya kutumia mali yangu sawa ninavyotaka? Unapatwa na wivu kwa sababu mimi ni mwema?’ ”
Enyi watu! Musikilize vile mimi Yawe ninavyosema: Nimekuwa kama vile jangwa au inchi yenye giza kubwa? Kwa nini basi watu wangu wanasema: Sisi tuko watu huru; hatutakurudilia!
Yawe anasema hivi: Babu zenu waliona kosa gani kwangu hata wakanigeuka na kuniacha, wakakimbilia miungu ya bure, hata nao wakakuwa watu bure?
Naye Yawe akamujibu Yona: Unazani kwamba unafanya vema kukasirika?
Ukitenda vyema hautakubaliwa? Na usipotenda vyema, basi, zambi inajificha kwa mulango; inakutamani, lakini unapaswa kuishinda.”
Lakini Mungu akamwuliza Yona: Unazani unafanya vema kuukasirikia mumea huo? Yona akajibu: Ndiyo, ninafanya vema kukasirika – kukasirika hata kufa!