Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 4:26 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

26 Seti naye akapata mutoto mwanaume, akamwita Enosi. Hapo ndipo watu walipoanza kumwomba Yawe kwa jina lake.

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 4:26
17 Referans Kwoze  

Nitakutolea sadaka za shukrani. Nitaomba kwa jina la Yawe.


Kisha, wao watamwomba mungu wao, nami nitamwomba Yawe. Mungu atakayejibu kwa kuleta moto, yule ndiye Mungu wa kweli.” Na pale watu wote wakasema: “Sawa!”


Wakati huo nitabadilisha luga ya watu, nitawawezesha kusema luga safi kusudi waniite mimi Yawe, na kuniabudu kwa moyo mumoja.


Kisha Abramu akaondoka, akaelekea kwenye mulima upande wa mashariki ya Beteli akapiga hema kati ya muji wa Beteli, upande wa magaribi, na muji wa Ai upande wa mashariki. Pale vilevile akamujengea Yawe mazabahu na kumwomba kwa jina lake.


Wakati huo inchi ya Yuda itaokolewa na Yerusalema utakuwa salama. Na muji huo utaitwa “Yawe ni Ukombozi Wetu”.


Kwa hiyo, Isaka akajenga mazabahu kule na kumwabudu Yawe. Akapiga kambi kule, na watumishi wake wakachimba kisima.


Tunawaandikia ninyi kanisa la Mungu linalokuwa Korinto, ninyi ambao mumetakaswa kwa njia ya kuungana kwenu na Yesu Kristo na mumeitwa na Mungu kuwa watu wake. Vilevile barua hii ni kwa wote wanaoabudu jina la Bwana Yesu Kristo fasi zote, anayekuwa Bwana wao na Bwana wetu vilevile.


Ni kama vile Maandiko Matakatifu yanavyosema: “Kila mutu anayemusihi Bwana, ataokolewa.”


Naye alipomwona, akamuleta Antiokia. Na kwa muda wa mwaka muzima Barnaba na Saulo walikusanyika katika kanisa la kule na wakawafundisha watu wengi. Ni kule Antiokia ndiko wanafunzi waliitwa kwa mara ya kwanza jina la Wakristo.


Halafu watu wote watakaoomba kwa jina la Bwana ataokolewa.’


Tumekuwa kama watu ambao haujawatawala hata kidogo, kama watu ambao hawakujulikana kwa jina lako. Heri ungepasua mbingu ushuke chini, milima ingetetemeka mbele yako!


Musikilize, enyi watu wa Yakobo, enyi munaojulikana kwa jina la Israeli, ninyi munaokuwa wa uzao wa Yuda. Ninyi munaapa kwa jina la Yawe, na kudai kwamba munamwabudu Mungu wa Israeli; lakini hayo si ukweli wala sawa.


Mumoja atasema: “Mimi ni wa Yawe”, mwingine atajiita kwa jina la Yakobo, mwingine ataandika juu ya mukono wake: “Wa Yawe”, na kujitambulisha kwa jina la Israeli.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite