Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 4:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Kisha Kaina akaondoka mbele ya Yawe, akaenda kuishi katika inchi ya Nodi, upande wa mashariki wa Edeni.

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 4:16
19 Referans Kwoze  

Yawe aliwakasirikia sana watu wa Yerusalema na Yuda hata akawafukuza mbali naye. Zedekia alimwasi mufalme wa Babeli.


mimi nitawanyanyua na kuwatupilia mbali, wao wenyewe pamoja na muji niliowapa wao na babu zao.


Kwa hiyo Shetani akaondoka mbele ya Yawe, akamutesa Yobu kwa vidonda vikali tangia kwenye miguu yake mpaka kwenye kichwa chake.


Yawe aliwakasirikia sana watu wa Yerusalema na Yuda, hata akawafukuza mbali naye. Zedekia alimwasi mufalme wa Babeli.


Lakini Yawe aliwarehemu na kuwaonea huruma. Aliwaangalia kwa wema kwa sababu ya agano lake na Abrahamu, Isaka na Yakobo. Hakuwaangamiza wala hajawaachilia hata kidogo mpaka leo.


Watu waliposikia ngurumo na kuona umeme ukiwaka na kusikia sauti ya baragumu juu ya mulima uliokuwa unafuka moshi, wote wakaogopa na kutetemeka. Wote wakasimama mbali,


Angalia, leo umenifukuza kutoka udongo wenye mboleo na mbali nawe. Basi, nitakuwa mukimbizi na mwenye kutangatanga katika dunia, na yeyote atakayeniona ataniua.”


Magaribi mwanaume na muke wake wakasikia Yawe Mungu akitembea katika bustani, nao wakajificha kati ya miti ya bustani, Yawe Mungu asipate kuwaona.


Wao wenyewe wanaeleza namna mulivyotupokea wakati tulipofika kwenu na namna mulivyoacha kuabudu sanamu na kumurudilia Mungu. Mulifanya vile kusudi mumutumikie Mungu mwenye uzima na wa kweli


Neno alikuwa yuko katika dunia, nayo dunia iliumbwa kwa njia yake, lakini ijapokuwa vile haikumutambua.


Vitu vyote viliumbwa kwa njia yake, wala hakuna hata kitu kimoja kilichoumbwa pasipo yeye.


Halafu mutaanza kumwambia: ‘Sisi tulikula na kunywa pamoja nawe, na wewe ulifundisha katika barabara za muji wetu.’


Kwa maana pahali popote watu wawili au watatu wanapokusanyika kwa ajili ya jina langu, mimi ni pale katikati yao.”


Mungu asimame sasa, na waadui zake watawanyike! Wanaomuchukia wakimbie mbali naye!


Ee Mungu, uwaazibu kwa makosa yao, waanguke katika mipango yao wenyewe; uwafukuze inje kwa sababu ya zambi zao nyingi, kwa sababu wamekuasi wewe.


Hataona tena mitiririko ya asali na ya maziwa.


Yawe akamwambia Shetani: “Basi, unaweza kufanya vile unavyotaka juu ya mali yake. Lakini tu yeye mwenyewe usimuguse.” Basi, Shetani akaondoka mbele ya Yawe.


Kaina akalala na muke wake, naye muke wake akapata mimba, akazaa Enoki. Kaina akajenga muji akauita kwa jina la mwana wake Enoki.


Basi, Yona akasimama kwa kukimbilia Tarsisi, mbali na uso wa Yawe. Akaenda mpaka katika muji wa Yofa ambapo alikuta mashua moja iko tayari kwenda Tarsisi. Alilipa bei ya safari, akapanda ndani ya mashua, akasafiri pamoja na watu wengine kwenda Tarsisi, mbali na uso wa Yawe.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite