Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 4:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Unapolima udongo, hautakupatia tena mazao yake. Utakuwa mukimbizi na mwenye kutangatanga katika dunia.”

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 4:12
16 Referans Kwoze  

Kwa vile wamekataa kumusikiliza, Mungu wangu atawatupilia; wao watatangatanga kati ya mataifa.


Na kwa njia ya wamoja wenu watakaobaki nitaleta woga ndani ya moyo wao, katika inchi ya waadui zao hata jani linalopeperushwa litawakimbiza. Watakimbia kama mutu anayekimbia vita. Watakimbia na kuanguka hata kama hakuna mutu anayewafukuza.


Mutatumia nguvu zenu bure maana mashamba yenu hayatatoa mavuno na inchi yenu haitazaa matunda.


Kwa maana viumbe vyote vimewekwa chini ya utawala wa mambo ya ovyo, si kwa mapenzi yao, lakini kwa sababu ya yule aliyewatia katika hali hiyo. Lakini kungali tumaini hili:


Watoto wake watangetange na kuombaomba; wafukuzwe katika mabaki ya nyumba zao!


Angalia, leo umenifukuza kutoka udongo wenye mboleo na mbali nawe. Basi, nitakuwa mukimbizi na mwenye kutangatanga katika dunia, na yeyote atakayeniona ataniua.”


Kaina akamwambia Yawe: “Azabu yangu ni kubwa sana. Siwezi kuivumilia.


Mimi nitawashambulia, nanyi mutapigwa na waadui zenu. Mutatawaliwa na wale wanaowachukia. Mutatishwa na kukimbia hata kama hakuna mutu yeyote anayewafukuza.


“Lakini kama hamutaitii sauti ya Yawe, Mungu wenu, kama hamutakuwa waangalifu kushika amri zake zote na masharti ninayowaamuru leo, basi mutapatwa na laana hizi zote:


Mashamba yamebaki matupu. Inchi inaomboleza, maana ngano imeharibiwa, divai imetoweka, mafuta yamekosekana.


Udongo wenye mboleo akaugeuza kuwa udongo usioweza kutoa, kwa sababu ya uovu wa wakaaji wake.


Mutu anayelemewa na kosa ya kuua mutu, atakuwa mukimbizi mpaka katika kaburi. Mutu yeyote asijaribu kumusaidia.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite