Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 39:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Basi, Yosefu akapata kukubaliwa mbele ya Potifari, hata akakuwa mutumishi wake wa pekee. Akamufanya musimamizi wa nyumba yake na mwangalizi wa mali yake yote.

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 39:4
23 Referans Kwoze  

Mujichunge ninyi wenyewe na muchunge vilevile lile kundi lote Roho Mutakatifu alilowapatia kusudi mukuwe wasimamizi wao. Hivi mutaweza kuchunga kanisa la Mungu ambalo alijipatia kwa damu ya Mwana wake.


Anayetunza muti wa tini atakula matunda yake. Anayetumikia bwana wake ataheshimiwa.


Lakini Yosefu akakataa na kumwambia yule muke wa bwana wake: “Sikiliza! Bwana wangu amenipa mamlaka juu ya kila kitu hapa ndani ya nyumba na hajishugulishi na kitu chochote tena.


Siku moja Abrahamu akamwambia mutumishi wake aliyekuwa muzee kuliko wengine na musimamizi wa mali yake yote: “Weka mukono wako chini ya paja yangu,


Ni kweli kwamba mimi mutumishi wako nimepata kukubaliwa mbele yako, nawe umenitendea mema sana kwa kuokoa maisha yangu. Lakini kwenye milima ni mbali sana. Maangamizi haya yatanikuta mbele sijafika kule, nami nitakufa.


Kuna mutu mwenye akili na maarifa ndani ya kazi? Yule atawatumikia wafalme; hatawatumikia watu wasiofaa.


Mutumwa mwenye hekima atatwaa nafasi ya mwana mupumbafu. Atapata sehemu ya urizi wa jamaa hiyo.


Yawe akipendezwa na mwenendo wa mutu, anawageuza hata waadui zake kuwa warafiki.


Yakobo akamwambia: “Hapana! Kama kweli nimekubaliwa mbele yako, ninakusihi uipokee zawadi yangu. Hakika, kuona uso wako ni kama kuona uso wa Mungu, kwa vile ulivyonipokea kwa wema mukubwa.


na kusema: “Bwana wangu, nikipata kukubaliwa mbele yako, tafazali usinipite mimi mutumishi wako lakini ushinde kwangu.


Mufalme anapendezwa na mutumishi anayetenda kwa hekima, lakini hasira yake inawapata wanaotenda mambo yasiyofaa.


Halafu Saulo alituma ujumbe kwa Yese na kusema: “Umwache Daudi akae hapa anitumikie kwa sababu amepata kukubaliwa mbele yangu.”


Halafu Esau akauliza: “Kundi lile nililokutana nalo katika njia lina maana gani?” Yakobo akamujibu: “Nilitumaini kupata kukubaliwa mbele yako, ee bwana wangu.”


Akawapa maagizo haya: “Mutamwambia bwana wangu Esau hivi: Mutumishi wako Yakobo anasema hivi: ‘Nimekaa mugeni kwa Labani mpaka sasa.


Lakini Abramu akasema: “Ee Yawe, utanipa nini wakati ninaendelea kuishi bila mutoto, na murizi wangu ni Eliezeri wa Damasiki?


Jemadari wake Simuri ambaye alisimamia nusu ya kundi ya magari yake ya vita alimwasi. Siku moja, mufalme Ela alipokuwa kule Tirza katika nyumba ya Arsa aliyekuwa musimamizi wa nyumba ya kifalme, alikunywa, akalewa.


Yule kiongozi wa wavunaji akajibu: “Ni binti Mumoabu aliyekuja pamoja na Naomi kutoka katika inchi ya Moabu.


Mutoto Samweli aliendelea kukomaa, akazidi kupendwa na Yawe na watu.


Hegayi akapendezwa na Esteri hata kiasi cha kumupendelea. Bila kupoteza wakati, akamupa Esteri mafuta na chakula. Vilevile, akamuhamishia pahali pazuri kabisa katika nyumba hiyo ya wanawake, akamuchagulia wajakazi saba kutoka nyumba ya mufalme.


Hivyo utakubaliwa na kusifiwa, mbele ya Mungu na mbele ya wanadamu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite