Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 39:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Yawe alikuwa pamoja na Yosefu, akamufanikisha sana. Yosefu akakuwa anakaa katika nyumba ya bwana wake Mumisri.

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 39:2
32 Referans Kwoze  

Daudi alifanikiwa katika kila kitu alichofanya, maana Yawe alikuwa pamoja naye.


Akiniita, mimi nitamwitikia; akikuwa katika taabu nitakuwa pamoja naye, nitamwokoa na kumupa heshima.


Mbele ya watu hawa, nitakufanya sawa ukuta mugumu wa shaba. Watapigana nawe, lakini hawataweza kukushinda, maana, mimi niko pamoja nawe, nipate kukuokoa na kukukomboa. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Wao wakamujibu: “Tumeona wazi kwamba Yawe yuko pamoja nawe. Kwa hiyo, tunafikiri inafaa tufanye kiapo pamoja nawe na kufanya agano,


Wakati ule, Abimeleki pamoja na Fikoli, jemadari wa jeshi lake, akamwendea Abrahamu, akamwambia: “Mungu yuko pamoja nawe katika kila kitu unachofanya.


Mukipita katika maji, mimi nitakuwa pamoja nanyi; mukipita katika mito, haitawashinda nguvu. Mukitembea katika moto, hamutaungua; ulimi wa moto hautawaunguza.


Usiku uleule Yawe alimutokea na kumwambia: “Mimi ni Mungu wa baba yako Abrahamu. Usiogope; niko pamoja nawe. Nitakubariki na kuwazidisha wazao wako kwa ajili ya Abrahamu, mutumishi wangu.”


Basi, usiogope, mimi nipo pamoja nawe. Usifazaike, mimi ni Mungu wako. Nitakuimarisha na kukusaidia; nitakulinda kwa mukono wangu wa ushindi.


Huyo ni kama muti uliopandwa kando ya vijito, unaozaa matunda kwa wakati wake, na majani yake hayanyauki hata kidogo. Anafanikiwa katika yote anayofanya.


Mimi niko pamoja nawe, nitakulinda popote utakapoenda na kukurudisha katika inchi hii. Sitakuacha mpaka nitakapotimiza ahadi niliyokupa.”


Anasema: “Munyamaze na kujua kwamba mimi ni Mungu! Mimi ninatukuzwa katika mataifa yote; mimi ninatukuzwa katika ulimwengu wote!”


Mataifa yanakasirika na falme zinatikisika; Mungu ananguruma, nayo dunia inayeyuka.


Kijana mumoja kati ya watumishi akasema: “Nimemwona kijana mumoja wa Yese, wa muji wa Betelehemu. Kijana yule ana ujuzi wa kupiga kinubi. Yule kijana ni shujaa, hodari wa kupigana katika vita, ana hekima katika kusema na mwenye umbo zuri; Yawe yuko pamoja naye.”


Samweli aliendelea kukomaa na Yawe akakuwa pamoja naye, na yale yote aliyosema hakuna hata moja ambalo halikutimia.


Lakini Saulo alipoona wazi kwamba Yawe alikuwa pamoja na Daudi, na kwamba Mikali binti yake alimupenda sana Daudi,


Watu wote wanaokuwa watumwa wanapaswa kuwaheshimu wabwana wao kabisa, kusudi watu wasitukane jina la Mungu na kuzarau mafundisho yetu.


“Angalia bikira atapata mimba, atazaa mutoto mwanaume, naye ataitwa Emanueli,” (maana yake “Mungu yuko pamoja nasi”).


Naye akamujibu: “Nitayaelewa namna gani pasipo mutu wa kunielezea?” Halafu akamwomba Filipo apande na kuikaa karibu naye ndani ya gari.


Mungu akakuwa pamoja na yule mutoto, naye akaendelea kukomaa. Alikaa katika jangwa na akakuwa mupiga upinde hodari sana.


Yule bwana wake akatambua kwamba Yawe alikuwa pamoja na Yosefu, na kwamba ndiye aliyefanikisha mambo yote Yosefu aliyofanya.


Yule mukubwa wa kifungo hakujishugulisha tena na kitu chochote Yosefu alichopewa kwa maana Yawe alikuwa pamoja na Yosefu na kufanikisha kila kitu alichofanya.


Basi, Yawe alikuwa pamoja na Yoshua na sifa zake zikaenea katika inchi yote.


Basi, Yawe alikuwa pamoja naye, na alimwezesha kwa kila jambo alilotenda. Alimwasi mufalme wa Asuria na kukataa kumutumikia.


Hakuna mutu atakayekushinda siku zote za maisha yako. Nitakuwa pamoja nawe kama nilivyokuwa pamoja na Musa. Siku zote nitakuwa nawe wala sitakuacha hata kidogo.


Kumbuka kwamba mimi nimekuamuru ukuwe imara na hodari. Usiogope wala usifazaike kwa sababu mimi Yawe, Mungu wako, niko pamoja nawe popote utakapoenda.”


Finehasi mwana wa Eleazari, alikuwa musimamizi wao, zamani, Yawe alikuwa pamoja naye.


Solomono, mwana wa mufalme Daudi, alijiimarisha katika utawala wake, naye Yawe, Mungu wake akamubariki na kumufanya akuwe mukubwa sana.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite