Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 39:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Basi, muke wa Potifari akamushika nguo yake na kumwambia: “Lala na mimi!” Lakini Yosefu akamwachia nguo yake katika mikono yake, akakimbilia inje.

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 39:12
16 Referans Kwoze  

Ujiepushe na tamaa za ujana, utafute kuishi katika haki, imani, upendo na amani pamoja na watu wote wanaomwabudu Bwana kwa moyo safi.


Wapendwa wangu, ninawasihi ninyi, kama vile wageni na wasafiri hapa katika dunia, muepuke tamaa za mwili zinazopigana na roho.


Jambo moja nililotambua linalokuwa baya zaidi kuliko kifo, ni mwanamuke ambaye moyo wake ni mutego na wavu, na mikono yake ni kama minyororo. Lakini anayemupendeza Mungu anamwepuka mwanamuke yule, lakini mwenye zambi ananaswa naye.


Ujiokoe kwa kujitoa katika mutego ule, ujiponyeshe kama vile paa au ndege anayemutoroka mwindaji.


Uepushe njia yako mbali naye, wala usiukaribie mulango wa nyumba yake,


Musidanganyike: “Warafiki wabaya wanaharibu tabia nzuri za watu.”


Yule mwanamuke akaendelea kumushawishi Yosefu siku kwa siku, lakini Yosefu hakumusikiliza wala kukubali kulala naye.


Lakini Yosefu akakataa na kumwambia yule muke wa bwana wake: “Sikiliza! Bwana wangu amenipa mamlaka juu ya kila kitu hapa ndani ya nyumba na hajishugulishi na kitu chochote tena.


Wewe mwana wangu usiandamane nao, uzuie muguu wako usifuatane nao.


Samweli alipogeuka kusudi aende zake, Saulo akashika pindo la nguo yake, nayo ikapasuka.


Siku moja, Yosefu akaingia ndani ya nyumba kufanya kazi yake kama kawaida, na watumishi wengine hawakukuwa ndani ya nyumba.


Kwa hiyo, yule mwanamuke alipoona kwamba Yosefu ameacha nguo yake katika mikono yake na kukimbilia inje,


Hapo, alipokuwa anamupatia mikate ile, Amunoni alimukamata na kumwambia: “Kuja ulale nami.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite