Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 34:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Muniombe mali na zawadi, hata ikiwa kikubwa namna gani, nami nitatoa, kufuatana na jinsi mutakavyoniambia. Lakini munipatie tu binti huyu kuwa muke wangu.”

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 34:12
13 Referans Kwoze  

Lakini wao wakamujibu: “Hapa tuko tu na mikate mitano na samaki mbili.”


Daudi vilevile alituma wajumbe kwa Isiboseti mwana wa Saulo akisema: “Unirudishie muke wangu Mikali ambaye nilimwoa kwa magovi mia moja ya Wafilistini.”


Kwa miaka makumi mbili hii yote nimeishi katika nyumba yako. Nilikutumikia miaka kumi na mine kwa ajili ya wabinti zako wawili, na miaka sita nikachunga nyama wako. Lakini wewe, ukabadilisha mushahara wangu mara kumi.


Yakobo akamupenda Rakeli; kwa hiyo akamwambia Labani: “Nitakutumikia miaka saba kwa ajili ya Rakeli, binti yako mudogo.”


Kisha akatoa vyombo vya feza na zahabu na nguo, akamupa Rebeka. Vilevile aliwapa wandugu na mama ya Rebeka mapambo ya bei kubwa.


Basi, nikamupata huyo mwanamuke kwa vikoroti kumi na vitano vya feza na saki nyingi za shayiri.


Vilevile, Sekemu akawaambia baba na wandugu za Dina: “Ninataka kukubaliwa mbele yenu, nami nitawapa ninyi chochote mutakachosema.


Basi, wana wa Yakobo wakamujibu Sekemu na baba yake Hamori kwa udanganyifu, kwa sababu Sekemu alikuwa amekwisha kumuchafua dada yao Dina.


Basi, watumishi hao wa Saulo walimwambia Daudi maneno hayo kwa siri, naye akawaambia: “Munazani mufalme kuwa baba mukwe wangu ni jambo dogo? Mimi ni mutu masikini na wa hali ya chini.”


Mutu akimutongoza binti ambaye hajachumbiwa, akilala naye, hakika atalipa mali na kumwoa binti yule.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite