Kisha Yawe wa majeshi akasema hivi: Hao watakuwa watu wangu. Watakuwa urizi wangu wa kipekee siku ile nitakaposimama kufanya jambo ninalokusudia. Sitawazuru kama vile baba asivyomuzuru mwana wake anayemutumikia.
Basi, Yakobo akainua macho, akamwona Esau akikuja pamoja na watu mia ine. Halafu, akawagawanya watoto wake kati ya Lea, Rakeli na wale wajakazi wawili.
lakini inchi yenu ya kuzaliwa itapatishwa haya; hiyo inchi mama yenu, itafezeheshwa. Babeli itakuwa ya mwisho kati ya mataifa, itakuwa mbuga yenye kukauka na jangwa.