Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 32:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Hao wajumbe walikwenda, kisha wakarudi na kumwambia Yakobo: “Tumefika kwa ndugu yako Esau, naye yuko katika njia kuja kukupokea, akiwa na watu mia ine.”

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 32:7
22 Referans Kwoze  

Kisha, tutakwenda Beteli kusudi nimujengee Mungu mazabahu, Mungu ambaye alinisaidia siku ya taabu na kuwa nami popote nilipokwenda.”


Nao wote wanaotaka kuishi maisha ya kumwabudu Mungu katika kuungana na Kristo Yesu, watateswa.


Yeye anatufariji katika taabu yetu yote, kusudi tupate kuwafariji wale wanaokuwa katika taabu yoyote kwa kuwaletea faraja tuliyopokea kutoka kwa Mungu.


Kule waliwajenga wanafunzi moyo na kuwatia nguvu wabakie katika imani wakiwaambia: “Ni sherti tupite katika mateso mengi kwa kuweza kuingia katika Ufalme wa Mungu.”


Nimewaambia maneno haya kusudi mukuwe na amani, mukibaki katika umoja nami. Mutapata mateso katika dunia. Lakini mujipe moyo, kwa kuwa mimi nimepata ushindi juu ya vyote katika dunia.”


“Muangalie! Ninawatuma kama kondoo katikati ya imbwa wa pori. Basi mukuwe waangalifu kama nyoka na wakamilifu kama njiwa.


Yesu akawajibu: “Sababu gani munaogopa kama hivi? Hakika imani yenu ni ndogo!” Halafu akasimama, akakaripia zoruba na maji na kukakuwa kimya kabisa ndani ya ziwa.


Mutu huyo anajua kufanya vile, kwa sababu Mungu wake anamufundisha.


Hekima itakulinda, ufahamu utakuchunga;


Roho yangu inaporegea kabisa, yeye yuko, anajua mwenendo wangu. Waadui wamenitegea mitego katika njia ninayopita.


Halafu katika taabu yao wakamulilia Yawe, naye akawaokoa katika mateso yao.


Usikie kilio changu, ee Mungu, usikilize maombi yangu.


Nimesahaulika kama mutu aliyekufa; nimekuwa kama chungu kilichovunjikavunjika.


Waisraeli walipoinua macho na kumwona mufalme wa Misri akikuja na jeshi lake nyuma yao, wakashikwa na hofu kubwa, wakamulilia Yawe.


sistahili hata kidogo wema wote na uaminifu wote ulionitendea mimi mutumishi wako. Nilipovuka muto Yordani, sikukuwa na kitu isipokuwa fimbo; lakini sasa nina makundi haya mawili.


Mutu muzuri anakopesha bila faida; anafanya shuguli zake kwa kutumia haki.


Yakobo alipowaona, akasema: “Hii ni kambi ya jeshi la Mungu!” Kwa hiyo akaita pahali pale “Kambi mbili”.


Basi, Yakobo akaogopa sana na kufazaika. Akawagawanya katika makundi mawili watu waliokuwa pamoja naye, kondoo, nyama wengine na ngamia,


Basi, Yakobo akainua macho, akamwona Esau akikuja pamoja na watu mia ine. Halafu, akawagawanya watoto wake kati ya Lea, Rakeli na wale wajakazi wawili.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite