Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 3:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Nitaweka uadui kati yako na yule mwanamuke, kati ya uzao wako na uzao wake. Yeye ataponda kichwa chako, nawe utamwuma kisigino chake.”

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 3:15
48 Referans Kwoze  

Mungu, anayeleta amani, atamupondaponda sasa hivi Shetani chini ya miguu yenu. Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo ikuwe pamoja nanyi.


Mutu anayefanya zambi ni mutu wa Shetani, kwa maana Shetani anafanya zambi tangia mwanzo wa vitu vyote. Kwa sababu hii, Mwana wa Mungu alikuja kusudi aharibu kazi za Shetani.


Yule nyoka akamukasirikia yule mwanamuke na kwenda kufanya vita na wazao wake wengine; ndio wale wanaoshika amri za Mungu na kufuata ukweli ulioshuhudiwa na Yesu Kristo.


Basi, Bwana mwenyewe atawapa kitambulisho: bikira atapata mimba, atazaa mutoto mwanaume na kumwita jina lake “Emanueli – Mungu Yuko Pamoja Nasi”.


Lakini wakati uliopangwa ulipotimia, Mungu akamutuma Mwana wake: akazaliwa na mwanamuke na kuishi chini ya uongozi wa Sheria,


Baba yenu ni Shetani, nanyi munataka kutimiza sawa vile huyo baba yenu anavyotamani. Yeye ni mwuaji siku zote, naye hajasimama katika ukweli, kwa sababu ndani yake hakuna ukweli. Wakati anaposema uongo, masemi yake yanatokana na tabia yake, kwa sababu yeye ni mwongo na baba ya uongo.


“Angalia bikira atapata mimba, atazaa mutoto mwanaume, naye ataitwa Emanueli,” (maana yake “Mungu yuko pamoja nasi”).


Shamba ni dunia. Mbegu nzuri ni washiriki wa Ufalme. Nyasi ni washiriki wa yule Mwovu Shetani.


Hii ndiyo njia inayoonyesha wazi tofauti kati ya watoto wa Mungu na watoto wa Shetani. Mutu asiyetenda mambo ya haki au asiyemupenda ndugu yake si mutoto wa Mungu.


Muangalie, nimewapa uwezo wa kukanyaga nyoka na nge na mamlaka ya kumushinda yule adui Shetani; wala hakuna kitu chochote kitakachowazuru.


Yawe alimwapia Daudi kiapo cha hakika, kiapo hiki ambacho hatakivunja: “Nitamuweka mumoja wa wazao wako mwenyewe, kuwa mufalme nyuma yako.


Kisha yule Mwovu aliyewadanganya, akatupwa katika ziwa la moto na lenye mawe ya kiberiti yanayowaka moto, pahali yule nyama wa ajabu na yule nabii wa uongo wanapokuwa. Nao watateswa muchana na usiku, milele na milele.


Mungu alinyanganya uwezo wa wakubwa na wenye mamlaka, naye akawaonyesha waziwazi, akiwatembeza kama wafungwa katika maandamano ya ushindi wa Mwana wake.


na kusema: “Wewe mutoto wa Shetani unayejaa udanganyifu na ukorofi wa kila namna! Wewe usiyependa kuona jambo la haki! Wewe hauchoki na kugeuza maneno ya ukweli ya Bwana!


Usiogope mateso utakayopata. Sikiliza, Shetani atawajaribu kwa njia ya kuwatia wamoja wenu katika kifungo, nanyi mutateseka kwa muda wa siku kumi. Lakini ukuwe mwaminifu mpaka kufa, nami nitakupatia taji ya uzima.


Kwa hiyo nitamugawanyia sehemu pamoja na wakubwa, atagawanya vitu vilivyotekwa pamoja na wenye nguvu. Alijitoa yeye mwenyewe hata kufa; aliwekwa kundi moja na watu wakosaji. Alizibeba zambi za watu wengi, akawaombea musamaha hao wakosaji.


Huyo mutawala atawachunga watu wake kwa nguvu ya Yawe, kwa utukufu wa Yawe, Mungu wake. Watu wake wataishi kwa usalama, maana atakuwa mukubwa mpaka kwa miisho ya dunia.


Utasitasita mpaka wakati gani, ewe binti usiyekuwa mwaminifu? Maana, mimi nimefanya kitu kipya katika dunia; mwanamuke anamulinda mwanaume.


Ni nani anayeshinda dunia? Ni yule anayeamini kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu.


Na kwa sababu yeye mwenyewe alijaribiwa na kuteswa, anaweza kuwasaidia wale wanaojaribiwa.


Kama vile Maandiko Matakatifu yanavyosema: “Alipopanda juu, alikamata wafungwa, aliwapatia watu zawadi.”


Akapewa ruhusa ya kupigana vita na watu wa Mungu na kuwashinda. Akapewa hata mamlaka ya kutawala watu wote, wa kila kabila, kila jamaa, kila luga na kila taifa.


Wakati Yesu alipoishi katika dunia, aliomba na kusihi kwa malalamiko makubwa pamoja na kutoa machozi kwa Mungu ambaye angeweza kumwokoa toka katika kifo. Mungu alimusikia Yesu kwa sababu yeye alimuheshimu.


Siku zote nilipokuwa pamoja nanyi katika hekalu, ninyi hamukunikamata. Lakini hii ni saa yenu; saa ya utawala wa bwana wa giza.”


Ninyi kikundi cha nyoka! Namna gani mutaweza kuepuka azabu ya jehenamu?


Ninyi kikundi cha nyoka! Namna gani ninyi munaokuwa wabaya, munaweza kusema maneno mazuri? Kwa maana kinywa kinasema maneno yanayojaa ndani ya moyo.


Yoane alipoona Wafarisayo wengi na Wasadukayo wakimufikia kwa kubatizwa, aliwaambia: “Ninyi kikundi cha nyoka! Ni nani aliyewaambia kwamba munaweza kuponyoka azabu ya Mungu inayokaribia?


Vinywa vyao ni kama kaburi wazi, ndimi zao ni za kudanganya, ndani ya midomo yao munatoka sumu kali sawa ya nyoka.


Na wewe, mutoto wangu, utaitwa nabii wa Mungu Mukubwa, maana utatangulia mbele ya kufika kwa Bwana, kusudi umutengenezee njia.


wakishika nyoka au kunywa sumu yoyote, hawatakufa. Wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapona.”


Lakini hakulala naye mpaka alipozaa yule mutoto mwanaume. Yosefu akamwita jina lake Yesu.


Atakuwa kama nyoka katika njia, nyoka mwenye sumu kando ya njia, anayeuma visigino vya farasi, naye mupanda-farasi anaanguka machali.


Kisha majuma hayo makumi saba na mawili, yule aliyepakwa mafuta atauawa na hatabaki na kitu. Muji na Pahali Patakatifu Sana vitaharibishwa na waaskari wa mutawala atakayekuja kushambulia. Mwisho wake utafika kama mafuriko, kukiwa vita na maangamizi kama yalivyopangwa na Mungu.


Hata wakijificha juu ya mulima Karmeli, huko nitawatafuta na kuwakamata; hata wakijificha mbali nami katika vilindi vya bahari, mule nitaiamuru nyoka kubwa ya bahari iwaume.


Kisha akawaelezea maneno yaliyoandikwa juu yake katika Maandiko Matakatifu yote, akianza toka vitabu vya Musa na kuendelea katika vitabu vya manabii wote.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite