Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 3:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Kisha Yawe akamwambia nyoka: “Kwa sababu umefanya hivyo, umelaaniwa kuliko nyama wote wa kufugwa, na kuliko nyama wote wa pori. Utatambaa kwa tumbo lako na kula mavumbi siku zote za maisha yako.

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 3:14
10 Referans Kwoze  

Watatambaa katika mavumbi kama nyoka, kama viumbe vinavyotambaa. Watatoka katika makimbilio yao wakitetemeka na kujaa hofu. Watakugeukia Yawe, Mungu wetu, kwa hofu, wataogopa kwa sababu yako.


Imbwa wa pori na kondoo watakula pamoja, simba watakula majani kama ngombe, lakini chakula cha nyoka kitakuwa mavumbi. Katika mulima wangu wote mutakatifu, hakuna atakayeumiza au kuharibu kitu. –Ni Yawe anayesema hivyo.


Waadui zake wanaokaa katika jangwa wanyenyekee mbele yake, wapinzani wake walambule vumbi.


Utaangushwa mbali sana ndani ya udongo, kutoka kule mbali utatoa sauti, maneno yako yatatoka kule chini katika mavumbi, sauti yako itatoka ndani ya udongo kama ya muzimu.


Kwa hiyo, munapaswa kutia tofauti kati ya nyama asiyekuwa muchafu na anayekuwa muchafu, kati ya ndege asiyekuwa muchafu na anayekuwa muchafu. Musijichafue kwa kugusa nyama au ndege au chochote kinachotambaa juu ya udongo ambacho nimekitenga kuwa ni kichafu.


Anayemwanga damu ya mwanadamu, damu yake itamwangwa na mwanadamu; maana mwanadamu aliumbwa kwa mufano wa Mungu.


Nyoka alikuwa mwerevu kuliko nyama wote wa pori walioumbwa na Yawe Mungu. Basi, nyoka akamwambia yule mwanamuke: “Ni kweli Mungu alisema musikule matunda ya muti wowote katika bustani?”


Sasa wewe unalaaniwa juu ya udongo ambao ulifungua kinywa kwa kupokea damu ya ndugu yako uliyemwua.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite