6 Esau akatambua kwamba Isaka alibariki Yakobo na kumutuma aende kuoa kule Padani-Aramu, na kwamba alipomubariki, alimukataza asioe mwanamuke Mukanana.
Hivyo Isaka akamwita Yakobo, akamubariki, akamwagiza akisema: “Usioe mwanamuke yeyote Mukanana.
Hapo Isaka akatetemeka sana, akasema: “Ni nani basi yule aliyewinda na kuniletea nyama ya mawindo, nami nimekwisha kula mbele haujakuja? Tena nimekwisha kumubariki. Hakika, amekwisha kubarikiwa!”
Isaka alipokuwa na umri wa miaka makumi ine akamwoa Rebeka, binti ya Betueli, Musuria wa Padani-Aramu. Rebeka alikuwa dada ya Labani.
Akatambua vilevile kwamba Yakobo alimutii mama yake na baba yake, akakwenda Padani-Aramu.