Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 27:41 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

41 Basi, Esau akamuchukia Yakobo kwa sababu ya baraka aliyokuwa amepewa na baba yake. Esau akawaza: “Siku za kilio cha baba zitakapokwisha, ndipo nitakapomwua ndugu yangu Yakobo.”

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 27:41
34 Referans Kwoze  

Lakini wandugu zake walipoona kwamba baba yao alimupenda Yosefu kuliko wao, wakamuchukia hata hawakuzungumuza naye kwa amani.


Usikuwe mwepesi wa hasira, maana, hasira inakaa ndani ya wapumbafu.


Akiwa amejaa mabaya ndani ya moyo, anatunga maovu. Anaamusha ugomvi kila pahali.


Wandugu zake wakamwuliza: “Unataka kutuambia kwamba utatutawala? Au utakuwa na mamlaka juu yetu?” Basi, wakazidi kumuchukia kwa sababu ya ndoto na maneno yake.


Nina ngombe, punda, makundi ya kondoo, watumwa na wajakazi. Ninakutumia ujumbe huu, bwana wangu, kusudi nipate kukubaliwa mbele yako.’ ”


Kwa maana zamani sisi vilevile tulikuwa wajinga, waasi na wapotovu. Tulikuwa tumetawaliwa na kila namna ya tamaa mbaya na ya vitu mbalimbali vilivyotuvuta sana. Tuliishi katika uovu na wivu, tuliwachukiza watu nao walituchukia.


Ulikuwa adui wa siku zote wa Waisraeli, ukasababisha watu wake wauawe kwa upanga, wakati wa musiba wao, wakati wa azabu yao ya mwisho.


Maana wao wako mbio kutenda maovu, haraka zao zote ni za kumwanga damu.


Ninamutolea malalamiko yangu, ninamwelezea taabu zangu.


Afazali mali kidogo ya mutu wa haki kuliko utajiri mwingi wa watu waovu.


Nikakuwa kama ninamulilia rafiki au ndugu yangu. Nilikwenda huku na huko kwa huzuni, kama mutu anayeomboleza kifo cha mama yake.


Basi watumishi wake walipomutoa katika gari lake la vita, wakamubeba na gari lake la pili mpaka Yerusalema. Naye akakufa na kuzikwa katika makaburi ya kifalme. Watu wote wa inchi ya Yuda na Yerusalema wakaomboleza kifo cha Yosia.


Waisraeli wakaomboleza kifo chake kwa muda wa siku makumi tatu kwenye inchi ya bonde la Moabu. Kisha siku za kilio na maombolezo ya kifo chake zikaisha.


akiwa muzee wa miaka mingi, akakufa na kukutana na wazee wake. Watoto wake, Esau na Yakobo wakamuzika.


sistahili hata kidogo wema wote na uaminifu wote ulionitendea mimi mutumishi wako. Nilipovuka muto Yordani, sikukuwa na kitu isipokuwa fimbo; lakini sasa nina makundi haya mawili.


Lakini Rebeka alipojua nia ya mwana wake mukubwa, akamwita mwana wake mudogo Yakobo, akamwambia: “Angalia, ndugu yako Esau anajifariji akikusudia kukuua.


Yakobo alipowaona, akasema: “Hii ni kambi ya jeshi la Mungu!” Kwa hiyo akaita pahali pale “Kambi mbili”.


Kisha, akawaagiza waganga wake wamupakae baba yake Israeli, dawa kusudi asioze, nao wakafanya hivyo.


Wandugu zake walipomwona akiwa mbali na mbele hajafika karibu, wakafanya mupango wa kumwua.


Nyuma ya kifo cha baba yao, wandugu za Yosefu walisemezana: “Labda Yosefu atatuchukia na kutulipiza mabaya yote tuliyomutendea.”


Ndugu aliyetendewa kosa ni mugumu kuliko muji wenye ukuta; magomvi yanakaza kama vile vifungio vya mulango wa ukuta.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite