Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 27:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Halafu unitengenezee chakula kitamu, kile ninachopenda, uniletee nikule, nipate kukubariki mbele ya kufa kwangu.”

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 27:4
23 Referans Kwoze  

Kwa njia ya imani, Isaka aliwabariki Yakobo na Esau kuelekea mambo ya siku zitakazokuja.


Yosefu akamujibu baba yake: “Hawa ni wana wangu Mungu alionijalia nikiwa huku.” Israeli akasema: “Tafazali, uwalete karibu nipate kuwabariki.”


Hayo ndiyo makabila kumi na mawili ya Israeli, na hayo ndiyo maneno baba yao aliyowaambia alipowabariki, kila mumoja wao kama alivyostahili.


Basi, baba yake akasema: “Uniletee hiyo nyama nikule mawindo yako mwana wangu, nikubariki.” Kwa hiyo Yakobo akamupelekea chakula, naye akakula; akamupelekea divai vilevile, akakunywa.


Alipokuwa akiwabariki akajitenga nao na kunyanyuliwa mbinguni.


Simeoni akawabariki na kumwambia Maria, mama yake: “Mutoto huyu amezaliwa kwa sababu ya kuwaangusha na kuwasimamisha watu wengi katika Israeli. Naye atakuwa kitambulisho kutoka kwa Mungu watu watakachokipinga,


Basi, Yoshua akawabariki na kuwaruhusu waende zao akawaambia:


Halafu Yoshua akamubariki Kalebu mwana wa Yefune na kumupa muji wa Hebroni kuwa sehemu yake.


amwindie nyama na kumutengenezea chakula kitamu, akikule, apate kumubariki mbele ya Yawe mbele ya kufa kwake.


Mungu Mwenye Nguvu akubariki upate wazao wengi na kuongezeka, kusudi ukuwe jamii kubwa ya watu.


Esau vilevile akatengeneza chakula kitamu, akamupelekea baba yake, akamwambia: “Basi baba, amuka ukule nyama ya mawindo yangu mimi mwana wako, upate kunibariki!”


Basi, Yakobo akamukaribia baba yake na kumubusu, na baba yake aliposikia harufu ya nguo zake, akamubariki akisema: “Hii ni harufu nzuri ya mwana wangu. Ni kama harufu ya shamba Yawe alilobariki!


Hakumutambua kwa sababu mikono yake ilikuwa yenye nywele nyingi kama ya Esau kaka yake; kwa hiyo akamubariki.


Basi, wakamubariki Rebeka wakisema: “Ewe dada yetu! Ukuwe mama wa maelfu kwa maelfu; wazao wako warizi miji ya waadui zao.”


akamubariki Abramu akisema: “Abramu abarikiwe na Mungu Mukubwa, Muumba wa mbingu na dunia!


Kumbe, Rebeka alikuwa anasikiliza wakati ule Isaka alipokuwa akiongea na Esau, mwana wake. Kwa hiyo, Esau alipokwenda katika pori kuwinda,


Kwenda kwenye kundi la mbuzi uniletee wana-mbuzi wawili wazuri, nimutengenezee baba yako chakula kitamu, kile anachopenda.


Basi, Yakobo akakwenda kutwaa wana-mbuzi wawili na kuwaletea kwa mama yake. Naye akatayarisha chakula kitamu sawa vile baba yake Isaka alivyopenda.


Kisha akamupa kile chakula kitamu na mukate aliokuwa ametayarisha.


Yakobo akamujibu baba yake: “Ni mimi Esau, muzaliwa wako wa kwanza. Nimefanya kama ulivyoniagiza. Tafazali baba, amuka uikae ukule nyama ya mawindo yangu kusudi upate kunibariki.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite