Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 26:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Ukae katika inchi hiyo, nami nitakuwa pamoja nawe na kukubariki. Nitatimiza ahadi niliyomupa baba yako Abrahamu, maana nitakupa wewe na wazao wako inchi hizi zote.

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 26:3
42 Referans Kwoze  

Mimi niko pamoja nawe, nitakulinda popote utakapoenda na kukurudisha katika inchi hii. Sitakuacha mpaka nitakapotimiza ahadi niliyokupa.”


Anashika agano alilofanya na Abrahamu, na ahadi aliyomwapia Isaka.


Abrahamu alisafiri toka kule na kuelekea eneo la Negebu, akafanya makao yake kati ya Kadesi na Suri, kisha akakwenda kukaa kwa muda kule Gerari.


Nitakupa wewe na wazao wako inchi hii ambamo unaishi kama mugeni. Ni kusema inchi yote ya Kanana ikuwe mali yenu milele; nami nitakuwa Mungu wao.”


Siku hiyo, Yawe akafanya agano na Abramu akisema: “Ninawapa wazao wako inchi hii, toka muto Nili wa Misri mpaka ule muto mukubwa wa Furati,


Basi, simama uitembelee inchi hii katika upana na urefu, maana nitakupa wewe inchi ile.”


Inchi hii yote unayoona nitakupa wewe na wazao wako ikuwe yenu milele.


Halafu Yawe akamutokea Abramu, akamwambia: “Nitawapa wazao wako inchi hii.” Basi, Abramu akajenga mazabahu kwa ajili ya Yawe aliyemutokea.


Kwa njia ya imani, aliishi kama vile mugeni katika inchi ile Mungu aliyomwahidi. Yeye alikuwa akiishi katika hema kama vile Isaka na Yakobo walivyoishi. Wao vilevile walishiriki pamoja naye ahadi ile ile ya Mungu.


Mushike mambo yote muliyojifunza na kupokea toka kwangu, nayo yote muliyosikia na kuona kwangu. Naye Mungu wa amani atakuwa pamoja nanyi.


Musiogope maana mimi nipo pamoja nanyi. Nitawarudisha wazao wenu toka mashariki, nitawakusanya ninyi kutoka magaribi.


Mukipita katika maji, mimi nitakuwa pamoja nanyi; mukipita katika mito, haitawashinda nguvu. Mukitembea katika moto, hamutaungua; ulimi wa moto hautawaunguza.


Mungu anasema: “Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayofuata. Nitakushauria kwa uangalifu mukubwa.


Yawe alikuwa pamoja na Yosefu na kumutendea mema, hata kumufanya apate kukubaliwa mbele ya mukubwa wa kifungo.


Yawe alikuwa pamoja na Yosefu, akamufanikisha sana. Yosefu akakuwa anakaa katika nyumba ya bwana wake Mumisri.


Alikuwa na makundi ya kondoo, ngombe na watumwa wengi. Kwa hiyo, Wafilistini wakamwonea wivu.


Mwaka ule Isaka akapanda mbegu katika inchi ile, akavuna mara mia zaidi, maana Yawe alimubariki,


Naye Mungu, kwa sababu alitaka kuonyesha wazi kwa wale watakaopokea ahadi kwamba yeye hawezi kubadilisha shauri lake hata kidogo, akaihakikisha kwa kiapo.


Utatuonyesha uaminifu na wema wako sisi wazao wa Abrahamu na wa Yakobo, kama ulivyowaahidi babu zetu tangu zamani.


Unapomwazibu mutu zambi zake kwa kumwadibisha, unaharibu kama nondo kile anachokipenda. Hakika, kila mwanadamu ni kama pumzi tu!


Nyuma ya kifo cha Abrahamu, Mungu alimubariki mwana wake Isaka. Naye Isaka akaishi karibu na kisima cha Beri-Lahai-Roi.


Usiku uleule Yawe alimutokea na kumwambia: “Mimi ni Mungu wa baba yako Abrahamu. Usiogope; niko pamoja nawe. Nitakubariki na kuwazidisha wazao wako kwa ajili ya Abrahamu, mutumishi wangu.”


Yawe alisimama juu ya ngazi hiyo, akamwambia: “Mimi ni Yawe, Mungu wa Abrahamu baba yako, na Mungu wa Isaka. Nitakupa inchi unayoilalia wewe na wazao wako.


Kisha Yawe akamwambia Yakobo: “Rudia katika inchi ya wazee wako na kwa jamaa yako, nami nitakuwa pamoja nawe.”


Inchi niliyowapa Abrahamu na Isaka nitakupa wewe na wazao wako.”


Kisha Israeli akamwambia Yosefu: “Kama vile unavyoona, mimi niko karibu kufa. Hata hivyo, Mungu atakuwa pamoja nanyi, na kuwarudisha katika inchi ya babu zenu.


Kisha Yosefu akawaambia wandugu zake: “Mimi sasa ninakaribia kufa. Lakini Mungu hakika atawafikia kwa kuwasaidia. Atawatoa katika inchi hii na kuwapeleka katika inchi aliyowaapia Abrahamu, Isaka na Yakobo.”


Tena nilifanya agano nao kwamba nitawapa inchi ya Kanana ambako waliishi kama wageni.


Nami nitawapeleka katika inchi ile niliyoapa kumupa Abrahamu, Isaka, na Yakobo. Nitawapa inchi hiyo ikuwe yenu. Mimi ni Yawe.’ ”


Inchi hii yote nimeiweka mbele yenu. Basi, muende kutwaa inchi hiyo ambayo mimi Yawe niliapa kuwapa wazee wenu Abrahamu, Isaka, Yakobo na wazao wao.’ ”


Kisha Yawe akamwambia Musa: “Hii ndiyo inchi ile niliyomwapia Abrahamu, Isaka na Yakobo kwamba nitawapa wazao wao. Nimekuonyesha uione kwa macho yako mwenyewe, lakini hautafika huko.”


Anashika agano alilofanya na Abrahamu, na ahadi aliyomwapia Isaka.


Mungu akamujibu: “Hapana. Muke wako Sara atakuzalia mutoto mwanaume, nawe utamwita Isaka. Nitaimarisha agano langu kwake na wazao wake, kuwa agano la milele.


Mungu akasikia kilio chao, naye akakumbuka agano alilofanya na Abrahamu, Isaka, na Yakobo.


Mungu akamwambia: “Hakika nitakuwa pamoja nawe. Utawatoa watu wa Israeli na kuja kuniabudu mimi Mungu juu ya mulima huu. Hicho kitakuwa kitambulisho kwamba ni mimi Mungu niliyekutuma wewe.”


Nitawafanya kuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wenu. Ninyi mutatambua kwamba mimi ni Yawe, Mungu wenu, niliyewatoa katika nira za Wamisri.


Mungu si mutu, hata aseme uongo, wala si mwanadamu, hata abadilishe nia yake! Ataahidi kitu na asikifanye, au kusema kitu asikitimize?


Yeye anashika agano lake milele, anatimiza ahadi zake kwa vizazi elfu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite