Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 24:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Mbele hajamaliza kuomba, mara moja Rebeka, binti ya Betueli mwana wa Milka, muke wa Nahori, ndugu ya Abrahamu, akafika akibeba mutungi wake kwenye bega.

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 24:15
22 Referans Kwoze  

Abramu na Nahori wakaoa. Muke wa Abramu aliitwa Sarai. Muke wa Nahori aliitwa Milka, binti ya Harani ambaye vilevile alikuwa baba ya Isika.


Hata mbele hawajaniita, mimi nitawaitikia; mbele hawajamaliza kusema, nitakuwa nimewajibu.


“Mbele sijamaliza kuomba ndani ya moyo wangu, mara tu Rebeka akafika na mutungi wake wa maji juu ya bega, akateremuka kwenye kisima na kuteka maji. Nami nikamwambia: ‘Tafazali unipe maji ya kunywa.’


Halafu mutaomba, nami Yawe nitawaitikia; mutalia kwa sauti kwa kuomba musaada, nami nitajibu hivi: Niko hapa! Kama mukiondoa mambo ya kitumwa, mukiacha kuzarau wengine na kusema maovu,


Ee Mungu, unastahili sifa huko Sayuni. Watu wanapaswa kukutimizia viapo vyao,


Ujiepushe na uovu, utende mazuri; utafute amani na kuifuatilia.


Basi, wabinti saba wa kuhani mumoja wa kule Midiani wakafika kuchota maji na kuwakunywesha kondoo na mbuzi wa baba yao.


Basi Ruta akaendelea kuokota masuke mpaka magaribi; na kisha kupepeta hiyo shayiri alipata kilo makumi tatu na zaidi.


Siku moja, Ruta wa Moabu akamwambia Naomi: “Muniruhusu niende kukusanya masalio ya mavuno pahali nitakapopata kukubaliwa na mwenye shamba.” Naomi akamwambia: “Basi, uende binti yangu.”


Yakobo alipokuwa bado anazungumuza na hao wachungaji, Rakeli akafika na kondoo wa baba yake, maana yeye ndiye aliyekuwa akiwachunga.


Rebeka akajibu: “Mimi ni binti ya Betueli mwana wa Milka, muke wa Nahori.


Hawa ndio wazao wa Tera, baba ya Abramu, Nahori na Harani. Harani alikuwa baba ya Loti.


Anachunguza yote yanayofanyika katika nyumba yake; hakai bure hata kidogo.


Hivyo, asubui mapema, Abrahamu akatwaa chakula na chupa la maji, akamupa Hagari na kumubebesha mutoto juu ya bega. Akamufukuza pamoja na mwana wake. Hagari akaondoka, akakuwa anatangatanga katika jangwa la Beri-Seba.


Basi, binti nitakayemwambia atue mutungi wake wa maji anipatie maji nikunywe, naye akinipa mimi na kuwakunywesha ngamia wangu, akuwe ndiye uliyemuchagulia mutumishi wako Isaka. Jambo hilo litanionyesha kwamba umemutendea mema bwana wangu.”


Isaka alipokuwa na umri wa miaka makumi ine akamwoa Rebeka, binti ya Betueli, Musuria wa Padani-Aramu. Rebeka alikuwa dada ya Labani.


Walipokuwa wanapanda mulima kuelekea katika muji, wakakutana na wabinti waliokuwa wakienda kuteka maji. Wakawauliza wabinti wale: “Mwonaji yuko katika muji?”


Naye akawauliza: “Munamufahamu Labani mwana wa Nahori?” Wakamujibu: “Tunamufahamu.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite