Mwanzo 23:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
9 aniuzishie lile pango lake la Makipela linalokuwa kwa mupaka wa shamba lake. Mumusihi aniuzishie nilifanye makaburi yangu. Anipatie kwa bei ya haki hapahapa mbele yenu.”
Efuroni mwenyewe alikuwa kati ya Wahiti hao waliokuwa wamekutanika kwenye mulango wa muji. Basi, Efuroni Muhiti, akamujibu Abrahamu mbele ya Wahiti wote pale kwenye mulango:
Kisha Israeli akawaagiza wana wake hivi: “Mimi niko karibu kufa na kwenda kukutana na watu wangu. Munizike pamoja na wazee wangu katika pango linalokuwa katika shamba la Efuroni Muhiti,
wakamupeleka mpaka inchi ya Kanana, wakamuzika katika pango lililokuwa katika shamba kule Makipela, upande wa mashariki wa Mamure. Pango pamoja na shamba lile Abrahamu alikuwa amelinunua kwa Efuroni Muhiti, kusudi pakuwe pahali pake pa kuzikia.
Daudi akamwambia Ornani: “Unipe nafasi ya uwanja wako wa kupepetea ngano kusudi nimujengee Yawe mazabahu juu yake, kusudi ugonjwa mukali upate kuzuiliwa katika watu. Uniuzishie kwa bei yake kamili.”
Lakini mufalme Daudi alimwambia Ornani: “Hapana; nitavinunua kwa bei yake kamili. Sitamutwalia Yawe kitu chako au kumutolea sadaka za kuteketezwa kwa moto ambazo sikununua.”