Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 23:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 aniuzishie lile pango lake la Makipela linalokuwa kwa mupaka wa shamba lake. Mumusihi aniuzishie nilifanye makaburi yangu. Anipatie kwa bei ya haki hapahapa mbele yenu.”

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 23:9
10 Referans Kwoze  

Musikuwe na deni la mutu yeyote. Deni moja munalopaswa kuwa nalo ni kupendana. Kwa maana yule anayemupenda mwenzake ametimiza Sheria kabisa.


Musimurudishie mutu ubaya kwa ubaya. Mukuwe na roho ya kufanya mema mbele ya watu wote.


“Mimi ninaishi kama mugeni kati yenu. Munipatie sehemu ya udongo ya kaburi, kusudi nipate kumuzika marehemu muke wangu.”


akawaambia: “Ikiwa munaniruhusu nimuzike marehemu muke wangu, tafazali mumwombe Efuroni mwana wa Sohari, kwa ajili yangu,


Efuroni mwenyewe alikuwa kati ya Wahiti hao waliokuwa wamekutanika kwenye mulango wa muji. Basi, Efuroni Muhiti, akamujibu Abrahamu mbele ya Wahiti wote pale kwenye mulango:


Abrahamu alikuwa amenunua shamba lile kwa Wahiti. Kule ndiko Abrahamu na muke wake Sara walizikwa.


Kisha Israeli akawaagiza wana wake hivi: “Mimi niko karibu kufa na kwenda kukutana na watu wangu. Munizike pamoja na wazee wangu katika pango linalokuwa katika shamba la Efuroni Muhiti,


wakamupeleka mpaka inchi ya Kanana, wakamuzika katika pango lililokuwa katika shamba kule Makipela, upande wa mashariki wa Mamure. Pango pamoja na shamba lile Abrahamu alikuwa amelinunua kwa Efuroni Muhiti, kusudi pakuwe pahali pake pa kuzikia.


Daudi akamwambia Ornani: “Unipe nafasi ya uwanja wako wa kupepetea ngano kusudi nimujengee Yawe mazabahu juu yake, kusudi ugonjwa mukali upate kuzuiliwa katika watu. Uniuzishie kwa bei yake kamili.”


Lakini mufalme Daudi alimwambia Ornani: “Hapana; nitavinunua kwa bei yake kamili. Sitamutwalia Yawe kitu chako au kumutolea sadaka za kuteketezwa kwa moto ambazo sikununua.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite