Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 23:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 “Mimi ninaishi kama mugeni kati yenu. Munipatie sehemu ya udongo ya kaburi, kusudi nipate kumuzika marehemu muke wangu.”

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 23:4
21 Referans Kwoze  

Kwa njia ya imani, aliishi kama vile mugeni katika inchi ile Mungu aliyomwahidi. Yeye alikuwa akiishi katika hema kama vile Isaka na Yakobo walivyoishi. Wao vilevile walishiriki pamoja naye ahadi ile ile ya Mungu.


Sisi tuko wageni mbele yako, na wasafiri kama vile babu zetu walivyokuwa wote. Siku zetu katika dunia ni kama kivuli kinachopita, hapa hakuna tumaini la kukaa.


Nitakupa wewe na wazao wako inchi hii ambamo unaishi kama mugeni. Ni kusema inchi yote ya Kanana ikuwe mali yenu milele; nami nitakuwa Mungu wao.”


Mimi ni mugeni tu hapa katika dunia; usinifiche amri zako.


Kule Mungu hakumupa Abrahamu hata sehemu ndogo ya shamba inayokuwa kama kikanyagio cha muguu kuwa urizi wake, lakini alimwahidi kwamba atamupa inchi hii kuwa urizi wake na wa wazao wake watakaoishi nyuma yake. Wakati ule, alikuwa hana mutoto.


Unapomwazibu mutu zambi zake kwa kumwadibisha, unaharibu kama nondo kile anachokipenda. Hakika, kila mwanadamu ni kama pumzi tu!


Musiuzishe mashamba kabisa, maana hiyo ni mali yangu na ninyi ni wageni na wasafiri katika inchi yangu.


kule Makipela, upande wa mashariki wa Mamure, katika inchi ya Kanana. Abrahamu alinunua pango na shamba hilo kwa Efuroni, Muhiti, likuwe lake la kuzikia.


Wapendwa wangu, ninawasihi ninyi, kama vile wageni na wasafiri hapa katika dunia, muepuke tamaa za mwili zinazopigana na roho.


mavumbi yanarudilia inchi tena, na roho inamurudilia Mungu aliyeipana.


watu wanaogopa mupando na kutishwa katika njia, muti wa lozi unachanua maua yake meupe, mapanzi hayawezi kuruka, hakuna hamu tena, mwanadamu anaelekea kwenye makao yake ya milele, waombolezaji wanasambaa katika njia,


Mutu akiweza kuzaa watoto mia moja, na akiishi maisha marefu, lakini kama mutu huyo hafurahii maisha yake, wala hafanyiwi mazishi, basi ninasema mutoto aliyezaliwa amekufa ni afazali kuliko mutu yule.


Kweli! Ninajua utanipeleka tu katika kifo, pahali wote wanaoishi watakapokutana.


wakamupeleka mpaka inchi ya Kanana, wakamuzika katika pango lililokuwa katika shamba kule Makipela, upande wa mashariki wa Mamure. Pango pamoja na shamba lile Abrahamu alikuwa amelinunua kwa Efuroni Muhiti, kusudi pakuwe pahali pake pa kuzikia.


Yakobo akamujibu: “Umri niliojaliwa kama musafiri ni miaka mia moja na makumi tatu. Miaka hiyo imekuwa michache na iliyojaa mateso, tena haijafikia hesabu ya miaka wazee wangu waliyoishi kama wasafiri.”


Kwa jasho la uso wako utajipatia chakula, mpaka utakaporudi katika udongo, maana ulitwaliwa katika udongo. Wewe ni mavumbi na utarudi katika mavumbi.”


Maiti zao zikapelekwa katika jimbo la Sekemu na kuzikwa katika kaburi lile Abrahamu alilonunua kwa feza kutoka kwa wazao wa Hemora.


Zipora akamuzalia mutoto mwanaume. Musa akasema: “Nimekimbilia katika inchi ya kigeni”, kwa hiyo akamupa yule mutoto jina Gersomi.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite