Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 23:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Abrahamu akakubaliana na Efuroni, akamupimia kadiri ya feza alizotaja mbele ya Wahiti wote, feza vikoroti mia ine, kadiri ya vipimo vya wachuuzi wa wakati ule.

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 23:16
18 Referans Kwoze  

Kisha nikawaambia: Kama mukipendezwa, munilipe mushahara wangu; lakini kama munaona sivyo, basi muache. Basi, wakanipimia vikoroti makumi tatu vya feza kwa mushahara wangu.


Nikalinunua shamba hilo linalokuwa kule Anatoti, kutoka kwa binamu yangu Hanameli, nikamulipa bei yake vikoroti kumi na saba vya feza.


Kuelekea maneno hayo, mutu yeyote asimukosee ndugu yake wala kumudanganya. Tumekwisha kuwaambia na kuwahakikishia mbele kwamba Bwana atawaazibu wale wanaofanya mambo kama hayo.


Kwa kumaliza, wandugu zangu, muweke mafikiri yenu juu ya mambo yote yanayokuwa ya kweli, ya heshima, ya haki, safi, ya kupendeza, nayo mambo yote yanayostahili sifa na ya utu wema.


Musikuwe na deni la mutu yeyote. Deni moja munalopaswa kuwa nalo ni kupendana. Kwa maana yule anayemupenda mwenzake ametimiza Sheria kabisa.


“Basi jambo lolote munalotaka wengine wawatendee, ninyi mulitende kwao vilevile, kwa maana kile ndicho kifungo cha Sheria ya Musa na mafundisho ya manabii.


Kwa kupima uzito: gera makumi mbili ni shekeli moja, shekeli makumi tano ni mina moja.


Hekima haiwezi kupatikana kwa zahabu, wala kwa kupima kiasi kingi cha feza.


Kila mumoja atakayehesabiwa anapaswa kulipa nusu ya shekeli kulingana na vipimo vya hema la mukutano. Hii ni sadaka yake atakayonitolea.


Tulipofika pahali pa kulala wageni kule katika njia, tukafungua mifuko yetu, tukashangaa kukuta feza ya kila mumoja wetu kwenye kinywa cha mufuko wake bila kuguswa. Sasa tumerudisha feza hiyo.


“Bwana, unisikilize. Shamba lenye bei ya vikoroti mia ine tu za feza ni nini kati yako na mimi? Umuzike marehemu muke wako.”


Maiti zao zikapelekwa katika jimbo la Sekemu na kuzikwa katika kaburi lile Abrahamu alilonunua kwa feza kutoka kwa wazao wa Hemora.


Kisha Israeli akawaagiza wana wake hivi: “Mimi niko karibu kufa na kwenda kukutana na watu wangu. Munizike pamoja na wazee wangu katika pango linalokuwa katika shamba la Efuroni Muhiti,


wakamupeleka mpaka inchi ya Kanana, wakamuzika katika pango lililokuwa katika shamba kule Makipela, upande wa mashariki wa Mamure. Pango pamoja na shamba lile Abrahamu alikuwa amelinunua kwa Efuroni Muhiti, kusudi pakuwe pahali pake pa kuzikia.


Kila mara alipokata nywele zake, (na kila mwisho wa mwaka alikata nywele zake maana zilikuwa nzito), alipozipima, zilikuwa na uzito wa kilo mbili kulingana na vipimo vya kifalme.


Nikatia sahihi juu ya barua ya ununuzi, nikaipiga muhuri, nikawaita washuhuda na kuipima ile feza juu ya mizani.


Lakini mufalme akamwambia Arauna: “Hapana! Wewe hautanipa kitu chochote. Mimi nitavinunua kwako kwa bei yake. Sitamutolea Yawe, Mungu wangu, sadaka za kuteketezwa ambazo sikununua.” Hivyo, mufalme Daudi alinunua kiwanja cha kupepetea na ngombe dume kwa bei ya vikoroti makumi tano vya feza.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite