Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 22:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Nyuma ya mambo yale, Mungu alimupima Abrahamu. Mungu alimwita: “Abrahamu!” Naye akaitika: “Niko hapa.”

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 22:1
24 Referans Kwoze  

Kwa njia ya imani, Abrahamu alimutoa Isaka kama vile sadaka wakati Mungu alipopima imani yake. Abrahamu alikubali kumutoa mwana wake wa pekee, ingawa ni yeye ndiye aliyekuwa amepewa ahadi na Mungu.


Mukumbuke jinsi Yawe, Mungu wenu, alivyowaongoza katika safari ndefu kupitia katika jangwa kwa muda wa miaka hiyo makumi ine, kusudi awanyenyekeze na kuwajaribu kusudi ajue yanayokuwa ndani ya mioyo yenu, na kama mungeshika amri zake au hapana.


Majaribu hayo ni kwa ajili ya kupima imani yenu. Zahabu ni kitu kinachoharibika, lakini ingawa vile inapimwa kwa njia ya kuchomwa ndani ya moto. Hivi vilevile imani yenu inayokuwa ya bei kali kuliko zahabu, inapaswa kupimwa kusudi ijulikane kuwa ya kweli. Na kwa sababu hii mutapata sifa, utukufu na heshima wakati Yesu Kristo atakapotokea.


Babu yetu Abrahamu alihesabiwa haki mbele ya Mungu kwa njia ya matendo yake. Yeye alimutoa mwana wake Isaka juu ya mazabahu.


Majaribu yale munayopata, ni yale yanayowapata watu wengine wote. Mungu hatawaachilia kujaribiwa kupita nguvu zenu, kwa maana yeye ni mwaminifu. Jaribu litakapowatokea, atawapatia nguvu ya kulivumilia, hata muweze kulishinda.


Zahabu na feza vinapimwa kwa moto, lakini Yawe ndiye anayepima mioyo ya watu.


Tena ni yeye aliyewakulisha mana katika jangwa, chakula ambacho babu zenu hawajapata kukijua. Alifanya hayo yote kusudi awanyenyekeze na kuwajaribu kwa kuwapima apate kuwajalia mema kwa mwisho.


Yawe alipoona kwamba Musa amegeuka kwa kuangalia kichaka, akamwita pale kutoka kichaka: “Musa! Musa!” Musa akaitika: “Niko hapa. Ninasikiliza!”


Lakini malaika wa Yawe akamwita kutoka mbinguni: “Abrahamu! Abrahamu!” Naye akaitika: “Niko hapa!”


Isaka akamwuliza baba yake: “Baba, tuko na moto na kuni. Lakini mwana-kondoo wa sadaka ya kuteketezwa yuko wapi?”


Kisha nikamusikia Yawe akisema: Nimutume nani? Ni nani atakayekuwa mujumbe wetu? Nami nikajibu: Niko hapa! Unitume mimi.


na hata wakati ambapo wajumbe wa wakubwa wa Babeli waliotumwa kwake kuuliza juu ya mambo ya ajabu yaliyotokea mule, Mungu, alimwacha ajiamulie mwenyewe, kusudi amupime na kujua yote yaliyokuwa ndani ya moyo wake.


Halafu Yawe akamwambia Musa: “Mimi nitawanyeshea mikate kutoka mbinguni. Kila siku watu watatoka na kukusanya chakula cha siku hiyo. Kwa njia hii nitawapima nione kama watafuata sheria zangu au hawatazifuata.


kisha neno, vitambulisho au maajabu aliyowaambia yakitokea, na akisema: ‘Tufuate miungu mingine, miungu ambayo hamujapata kuijua, na tuitumikie’,


Nitayatumia mataifa hayo kuwajaribu Waisraeli nione kama watairudilia njia yangu kama babu zao au sivyo.”


Kwa mara nyingine, Yawe aliwakasirikia Waisraeli, akamusukuma Daudi kuwatendea vibaya, akamwambia awahesabu watu wa Israeli na watu wa Yuda.


Yawe anawapima watu wa haki na waovu; anawachukia wanaopenda kutesa kwa ukali.


Nyuma ya mambo hayo, neno la Yawe lilimufikia Abramu katika maono kusema hivi: “Abramu! Usiogope! Mimi ni ngao yako. Zawadi yako itakuwa kubwa!”


Jambo hili lilimuhuzunisha sana Abrahamu kwa sababu Isimaeli vilevile alikuwa mutoto wake.


Basi, Israeli akamwambia Yosefu: “Unajua wandugu zako wanachunga nyama kule Sekemu. Kwa hiyo ninataka kukutuma kwao.” Yosefu akajibu: “Niko tayari.”


Mungu akaongea na Israeli katika maono usiku, akamwita: “Yakobo! Yakobo!” Yakobo akaitika: “Niko hapa.”


Halafu Yawe akamwita Samweli, naye Samweli, akaitika: “Niko hapa!”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite