Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 21:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Isaka alipotimiza umri wa siku nane, Abrahamu akamutahiri kama alivyoamuriwa na Mungu.

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 21:4
9 Referans Kwoze  

Halafu Mungu akafanya agano na Abrahamu, na kitambulisho cha kuhakikisha kwamba limeshikwa kilikuwa kutahiriwa. Kwa hiyo Abrahamu akamutahiri mwana wake Isaka alipotimiza siku nane za kuzaliwa. Naye Isaka akamutahiri mwana wake Yakobo, na Yakobo akawatahiri wana wake kumi na wawili waliokuwa babu zetu wakubwa.


Ilipotimia siku ya kumutahiri mutoto, ndiyo siku ya nane tangu alipozaliwa, wakamupa jina lake Yesu. Jina hili ni lile malaika alilojulisha mbele mama yake hajabeba mimba.


Ilipotimia siku nane tangu mutoto alipozaliwa, wakaenda kumutahiri, nao wakataka kumupa jina la baba yake Zakaria.


Wote wawili walikuwa wenye haki mbele ya Mungu, walishika kwa ukamilifu amri na maagizo yote ya Bwana.


Mutoto huyo atatahiriwa katika siku yake ya nane.


Mugeni yeyote anayeishi kati yenu akipenda kushiriki sikukuu ya Pasaka, anapaswa kwanza kutahiri wanaume wote wa nyumba yake. Halafu atahesabiwa kuwa kama mwenyeji na kuruhusiwa kushiriki. Mwanaume yeyote asiyetahiriwa asishiriki hata kidogo.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite