Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 20:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Lakini Mungu akamufikia Abimeleki katika ndoto usiku, akamwambia: “Wewe utakufa kwa sababu ya mwanamuke uliyemutwaa, maana yuko na mume wake.”

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 20:3
22 Referans Kwoze  

Pilato alipokuwa amekwisha kuikaa kwa kuamua maneno, muke wake akamutumia ujumbe huu: “Usijiingize katika maneno ya mutu huyo mwenye haki, kwa sababu usiku niliteseka sana katika ndoto kwa ajili yake.”


Sasa umurudishe yule mwanamuke kwa mume wake. Abrahamu ni nabii. Atakuombea nawe utaishi. Lakini usipomurudisha, ujue kwa hakika kwamba wewe utakufa pamoja na watu wako wote.”


Lakini Mungu hakuruhusu wateswe; kwa ajili yao aliwaonya wafalme, akisema:


Mungu anaongea na watu katika ndoto na maono, wakati usingizi muzito unapowapata,


Naye alipokuwa angali akifikiri juu ya maneno hayo, malaika wa Bwana akamutokea katika ndoto na kumwambia hivi: “Wewe Yosefu, mwana wa Daudi, usiogope kumwoa muchumba wako Maria, kwa maana mimba yake imetokana na uwezo wa Roho Mutakatifu.


Akaota ndoto, na katika ndoto hiyo, aliona ngazi iliyosimamishwa juu ya dunia na incha yake inafika mbinguni. Wamalaika wa Mungu walikuwa wakipanda na kushuka katika ngazi hiyo.


Alipofika, Yona aliingia katika muji. Kisha kutembea mwendo wa siku nzima, akaanza kutangaza: Kunabaki siku makumi ine tu na muji huu wa Ninawe utaangamizwa!


Wakamujibu: “Tuna huzuni kwa sababu tumeota ndoto na hakuna anayeweza kututafsiria ndoto zetu.” Yosefu akawaambia: “Kutafsiri ndoto si kazi ya Mungu? Basi, muniambie ndoto zenu.”


Kisha Yosefu akaota ndoto ingine, akawaelezea wandugu zake akisema: “Musikilize, nimeota ndoto nyingine. Nimeona jua, mwezi na nyota kumi na moja vinainamia mbele yangu.”


Usiku mumoja, Yosefu akaota ndoto, lakini alipowaelezea wandugu zake, wao wakazidi kumuchukia.


Lakini usiku, Mungu akamutokea Labani wa Aramu katika ndoto, akamwambia: “Ujichunge! Usimwambie Yakobo neno lolote, jema au baya.”


Lakini Yawe akamutesa na watu wote wa nyumba yake kwa mapigo makali kwa sababu ya Sarai, muke wa Abramu.


Mufalme akamwita Abramu, akamwuliza: “Ni kitu gani hiki ulichonitendea? Mbona haukunijulisha kwamba Sarai ni muke wako?


Kisha Mungu alimufikia Balamu, akamwuliza: Ni nani hawa wanaokaa nawe?


Mungu hakumuruhusu mutu yeyote awatese; kwa ajili yao aliwaonya wafalme:


Basi, usiku mumoja, yule mutunza vinywaji mukubwa na yule mupishi mukubwa wa mukate wa mufalme, waliota ndoto mule ndani ya gereza, kila mumoja na ndoto yake tofauti.


Mungu akaongea na Israeli katika maono usiku, akamwita: “Yakobo! Yakobo!” Yakobo akaitika: “Niko hapa.”


wapate kuachana na matendo yao mabaya, na kuvunja kiburi chao.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite