Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 2:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Halafu Yawe Mungu akamwumba mwanaume kwa udongo, akamupulizia ndani ya pua pumzi ya uzima, na yule mwanaume akakuwa kiumbe chenye uzima.

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 2:7
33 Referans Kwoze  

Kwa maana, Maandiko Matakatifu yanasema: “Mutu wa kwanza, Adamu, alikuwa kiumbe chenye uzima”; lakini Adamu wa mwisho ni Roho anayewapatia watu uzima.


Roho ya Mungu iliniumba, nayo pumzi ya Mungu Mwenye Uwezo inanipa uzima.


mavumbi yanarudilia inchi tena, na roho inamurudilia Mungu aliyeipana.


Usitukasirikie sana, ee Yawe, usiukumbuke uovu wetu siku zote! Ukumbuke kwamba sisi wote ni watu wako!


Yeye hahitaji kushugulikiwa na watu, kama vile angekuwa na lazima ya musaada fulani. Kwa maana yeye ndiye anayewapa watu wote pumzi ya uzima, pamoja na vitu vyote wanavyohitaji.


Adamu wa kwanza aliumbwa kwa udongo, yeye ni wa dunia, lakini Adamu wa pili alitoka mbinguni.


Kwa jasho la uso wako utajipatia chakula, mpaka utakaporudi katika udongo, maana ulitwaliwa katika udongo. Wewe ni mavumbi na utarudi katika mavumbi.”


ninaapa kwamba kadiri ninavyoweza kupumua, roho ya Mungu ikiwa bado ndani yangu,


kila kiumbe chenye uzima katika inchi kavu kilikufa.


Ujumbe wa Yawe unaoelekea Israeli. Yawe aliyezitandaza mbingu, aliyeiweka misingi ya dunia na kumupa mwanadamu uzima anasema hivi:


Mungu anajua jinsi tulivyoumbwa; anajua kwamba sisi ni mavumbi.


Mujue kwamba Yawe ndiye Mungu. Yeye ndiye aliyetuumba, sisi ni mali yake; sisi ni watu wake na kondoo wake anaowachunga.


Halafu sasa wewe mwanadamu ni nani hata ubishane na Mungu? Chombo cha udongo hakiwezi kumwuliza mufinyanzi: “Kwa nini umenitengeneza hivi?”


Usimutumainie mwanadamu, uzima wake ni kama pumzi tu. Yeye anafaa kitu gani?


Basi, Yawe Mungu akamufukuza Adamu inje ya bustani ya Edeni, kusudi alime udongo ambamo alitwaliwa.


Na ikiwa wababa zetu wa kimwili walituadibisha, nasi tuliwaheshimu, jambo hilo halionyeshi zaidi kwamba tunapaswa kumuheshimu Baba yetu wa kiroho na kupata kuishi?


Lakini Musa na Haruni wakajitupa uso mpaka chini na kusema: Ee Yawe unayekuwa asili ya uzima wa wanadamu wote. Mutu mumoja akikukosea, utakasirikia watu wote pamoja?


Zamiri ya mutu ni taa ya Yawe; inachunguza nafsi ya mutu mpaka ndani kabisa.


Wewe na mimi ni sawa mbele ya Mungu; mimi vilevile niliumbwa kwa sehemu ya udongo.


Kwa maana, tunajua kwamba hema hii tunayoishi ndani yake hapa katika dunia, maana yake mwili wetu, itakapobomolewa, Mungu atatupatia makao mengine mbinguni. Nayo ni nyumba aliyoijenga yeye mwenyewe na inayodumu milele.


Lakini sisi tunaokuwa na hazina hii ya kiroho, tuko vyombo vya udongo, kusudi watu waone waziwazi uwezo huu wa ajabu sana unaotoka kwa Mungu lakini si kwetu sisi wenyewe.


Alipokwisha kusema maneno haya, akawapulizia pumzi na kuwaambia: “Mupokee Roho Mutakatifu.


Zaidi sana wanadamu, viumbe vya udongo, watu ambao musingi wao ni mavumbi, ambao wanaweza kupondwapondwa kama chawa!


Ee Yawe, Mungu unayekuwa asili ya uzima wote, ninakuomba umuchague mutu wa kusimamia watu hawa,


wakati wa kupasua na wakati wa kushona, wakati wa kukaa kimya na wakati wa kusema,


Kwa maana, Adamu ndiye aliyeumbwa wa kwanza, na kisha Eva.


Maji yalitoka ndani ya udongo yakainywesha inchi yote.


Walimunasa yule ambaye maisha yetu yalimutegemea, yule mufalme aliyechaguliwa na Yawe yule ambaye tulisema juu yake: Chini ya ulinzi wake tutaishi kati ya mataifa.


Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitapulizia tena pumzi ndani yenu, nanyi mutaishi.


Mungu akaumba mutu kwa mufano wake. Ndiyo, kwa mufano wake Mungu alimwumba. Aliwaumba mwanaume na mwanamuke.


Nitawatia mishipa na nyama, nitawafunika ngozi na kutia pumzi ndani yenu, nanyi mutaishi. Hapo mutajua kwamba mimi ni Yawe.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite