Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 2:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 hakukukuwa mimea juu ya inchi wala miti haikukuwa imeota maana Yawe Mungu hakukuwa ameinyeshea inchi mvua, wala hakukukuwa mutu wa kuilima.

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 2:5
15 Referans Kwoze  

Basi, Yawe Mungu akamufukuza Adamu inje ya bustani ya Edeni, kusudi alime udongo ambamo alitwaliwa.


Udongo unaonyeshewa na mvua mara kwa mara na kutoa mimea inayofaa kwa walimaji, unabarikiwa na Mungu.


Ananyeshea inchi mvua, anapeleka maji katika mashamba.


Unapolima udongo, hautakupatia tena mazao yake. Utakuwa mukimbizi na mwenye kutangatanga katika dunia.”


Kisha akazaa ndugu yake Abeli. Abeli alikuwa mufugaji wa kondoo na Kaina alikuwa mulimaji.


Katikati ya miungu ya uongo ya mataifa nani anayeweza kunyesha mvua? Au, ni mbingu ndiyo inaweza kutoa manyunyu? Si ni wewe ee Yawe, Mungu wetu? Tunakuwekea wewe tumaini letu, maana ni wewe unayefanya haya yote.


Analeta mawingu kutoka miisho ya dunia, anapiga umeme na kunyesha mvua, anavumisha upepo kutoka gala zake.


Unaotesha majani kwa ajili ya mifugo, na mimea kwa matumizi ya mwanadamu kusudi naye apate chakula chake toka udongo:


Mufanye vile kusudi mupate kuwa kweli watoto wa Baba yenu anayekuwa mbinguni. Kwa maana yeye anawaangazia waovu na wema jua lake, naye anawanyeshea mvua wenye haki na wasiokuwa wenye haki.


Maji yalitoka ndani ya udongo yakainywesha inchi yote.


Yawe aliiumba dunia kwa nguvu zake; kwa hekima yake alisimamisha ulimwengu imara, kwa akili yake alizitandika mbingu juu.


Anapotoa sauti, maji yananguruma katika mbingu, anapandisha mawingu toka kwa miisho ya dunia. Anaufanya umeme upige wakati wa mvua, na kuuvumisha upepo katika gala zake.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite