Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 2:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Hivi ndivyo mbingu na dunia zilivyokamilika pamoja na vitu vyote vinavyokuwa ndani yake.

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 2:1
34 Referans Kwoze  

Mbingu ziliumbwa kwa neno la Yawe, na vyote vinavyokuwa ndani yake kwa pumzi ya kinywa chake.


Jambo hili litakuwa kitambulisho cha kudumu kati ya Waisraeli na mimi, maana mimi Yawe nilifanya mbingu na dunia kwa muda wa siku sita, lakini siku ya saba niliacha kufanya kazi, nikapumzika.


Maana kwa siku sita mimi Yawe niliumba mbingu na inchi, bahari na vyote vinavyokuwa ndani yake, kisha nikapumzika siku ya saba. Kwa hiyo mimi Yawe nilibariki siku ya Sabato, nikaitakasa.


Hapo mwanzo, Mungu aliumba mbingu na dunia.


Hivi ndivyo anavyosema Yawe aliyeumba mbingu, ndiye Mungu aliyeipa dunia umbo na kuifanya na kuiimarisha. Hakuiumba kusudi ibaki ukiwa, lakini aliipa umbo kusudi iikaliwe na viumbe vyake: Mimi ni Yawe, wala hakuna mwingine.


Hivi ndivyo anavyosema Yawe aliyeumba mbingu na kuzitandika kama hema, aliyeifanya dunia na vyote vinavyokuwa ndani yake, anayewapa watu wanaokaa ndani yake uzima, na kuwajalia uzima wote wanaoishi ndani yake:


Halafu akamwomba Yawe akisema: “Ee Yawe, Mungu wa Israeli, unayeikaa katika kiti cha kifalme juu ya makerubi, ni wewe tu unayekuwa Mungu, unayetawala falme zote za ulimwengu. Wewe uliumba dunia na mbingu.


Ni mimi niliyeifanya dunia, na kuumba mwanadamu anayeishi humo. Mikono yangu ndiyo iliyozitandaza mbingu, na kundi lote la nyota liko kwa amri yangu.


aliyeumba mbingu na dunia, bahari na vyote vinavyokuwa ndani yao. Yeye anashika ahadi yake milele.


Ujumbe wa Yawe unaoelekea Israeli. Yawe aliyezitandaza mbingu, aliyeiweka misingi ya dunia na kumupa mwanadamu uzima anasema hivi:


Maana alisema, na ulimwengu ukakuwa; alitoa amri, nao ukajitokeza.


Ezra akaomba akisema: Wewe peke yako ndiwe Yawe! Ulifanya mbingu na jeshi lake lote, dunia na vyote vinavyokuwa ndani yake, bahari na vyote vinavyokuwa ndani yake. Unavipatia uzima, na jeshi lote la mbinguni linakuabudu wewe.


Sasa ninakutumia fundi mwenye ujuzi sana na mwenye akili, jina lake Huruma-Abi.


Lakini sasa sisi tulioamini, tutaingia kwenye mapumziko ambayo Mungu alitaja aliposema: “Halafu nikaapa kwa kasirani kwamba hawataingia hata kidogo kwenye mapumziko niliyowatayarishia!” Mungu alisema vile ingawa alikuwa amemaliza kazi zake tangu pale alipoumba dunia.


Nao waliposikia habari hii, wote wakamwomba Mungu kwa nia moja, wakisema: “Ee Bwana, ni wewe uliyeumba mbingu, dunia na bahari na vitu vyote vinavyokuwa ndani yao.


Lakini Mungu wa Yakobo si kama sanamu hizo, maana, yeye ndiye aliyeumba vitu vyote, na Israeli ni taifa linalokuwa mali yake; Yawe wa majeshi, ndilo jina lake.


Yawe aliiumba dunia kwa nguvu zake; kwa hekima yake alisimamisha ulimwengu imara, kwa akili yake alizitandika mbingu juu.


Sasa, ninaumba mbingu mupya na dunia mupya. Mambo ya zamani hayatakumbukwa tena.


Kwa mukono wangu niliuweka musingi wa dunia, mimi mwenyewe nilizitandaza mbingu. Nikiziita mbingu na dunia, zinasimama haraka mbele yangu.


Mufanye angalisho kusudi wakati mutakapoangalia na kuona nyota, vitu vyote vya mbinguni, musivutwe kuviabudu na kuvitumikia. Vitu hivyo Yawe amewaachia watu wengine waviabudu.


Hivi ndivyo mbingu na dunia zilivyoumbwa. Siku ile Yawe Mungu alipoumba mbingu na dunia,


Mungu akapaita pahali pakavu “Inchi” na kusanyiko la maji akaliita “Bahari”. Mungu akaona kwamba ni vizuri.


naye amekwenda na kutumikia miungu mingine na kuiabudu, akiabudu jua, mwezi au vitu vingine vya mbinguni nisivyoagiza,


Itaachwa imetandazwa mbele ya jua na mwezi na nyota zote za mbingu, vitu ambavyo walivyopenda na kuvitumikia, na kuviendea kwa kuuliza shauri na kuviabudu. Mifupa hiyo haitakusanywa wala kuzikwa, lakini itabaki kama vile mboleo juu ya udongo.


Kama vile mbingu zinavyokuwa mbali na dunia, ndivyo njia zangu zinavyokuwa mbali na zenu, na mawazo yangu mbali na mawazo yenu.


Nani kati ya viumbe hivyo, asiyejua kwamba Yawe ametenda yale?


Basi Mungu akajitenga mbali nao, akawaacha waabudu nyota, jua na mwezi kufuatana na maneno haya yaliyoandikwa katika kitabu cha manabii: ‘Ninyi watu wa Israeli, si mimi muliyemuchinjia nyama na kumutolea sadaka zingine kwa muda wa ile miaka makumi ine katika jangwa.


Mara moja kukaonekana kundi kubwa la wamalaika kutoka mbinguni wakiwa pamoja na yule malaika, wakimutukuza Mungu na kusema:


Jeshi lote la anga litaharibika, anga zitakunjamana kama karatasi. Jeshi lake lote litanyauka, kama vile majani ya mizabibu au mitini yanavyonyauka.


Umejifunika mwangaza kama kanzu, umekunjua mbingu kama hema;


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite