Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




Mwanzo 19:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Lakini wao wakasema: “Utupitishe! Wewe ulikuja huku ukiwa mugeni na sasa unajifanya kuwa mwamuzi! Basi, tutakutendea mabaya zaidi ya wale wageni wako.” Halafu wakamusukuma Loti nyuma hata karibu wavunje mulango wake.

Gade chapit la Kopi




Mwanzo 19:9
21 Referans Kwoze  

Naye akamujibu: “Nani aliyekuweka wewe kuwa mukubwa na mwamuzi wetu? Unataka kuniua kama vile ulivyomwua yule Mumisri?” Kwa hiyo, Musa akaogopa na kufikiri: “Bila shaka jambo hilo limejulikana!”


Abramu akabaki katika inchi ya Kanana na Loti akakaa kati ya miji iliyokuwa katika bonde, akahamishia kambi yake Sodoma.


“Musiwape imbwa vitu vitakatifu, kusudi wasiwageukie na kuwararua, wala musiwatupie nguruwe ushanga zenu za bei kusudi wasizikanyagekanyage.


Walisikia haya walipotenda machukizo hayo? Hapana, hawakusikia haya hata kidogo. Hata zamiri hazikuwagonga. Kwa hiyo, wataanguka pamoja na wale walioanguka; nitakapowaazibu, wataangamia. –Ni Yawe anayesema hivyo.


Wao walisikia haya walipofanya machukizo hayo? Hapana! Hawakusikia haya hata kidogo. Hata zamiri hazikuwagonga. Kwa hiyo wataanguka pamoja na wale wanaoanguka; wakati nitakapowaazibu, wataangamizwa kabisa. –Ni Yawe anayesema hivyo.


Ndiyo maana manyunyu yamezuizwa kuanguka, wala mvua za mwisho hazijanyesha. Hata hivyo unakausha macho kama kahaba, wala hauna haya hata kidogo.


Wanawaambia wale wanaokutana nao hivi: Muikae mbali nami; musinikaribie kwa sababu mimi ni mutakatifu! Watu hao wananikasirikisha sana, hasira yangu ni kama moto usiozimika.


Mupumbafu anaanza kusema kwa maneno ya kijinga, na kumaliza masemi yake kwa wazimu wa hatari.


Hili ni jambo baya zaidi kati ya yote yanayotukia hapa chini ya jua, kwamba mwisho uleule unawapata wote. Tena, wakati wote wa maisha yao, wanadamu wanajaa uovu na wazimu, na kisha wanakufa.


Jiwe ni zito na muchanga vilevile, lakini uchokozi wa mupumbafu ni muzito zaidi.


Afazali kukutana na dubu dike aliyenyanganywa watoto wake, kuliko kukutana na mupumbafu katika upumbafu wake.


Mwenye hekima ni mwangalifu na anaepuka uovu, lakini mupumbafu hajizuizi wala hana uangalifu.


Sasa ufikiri juu ya jambo hili na uamue la kufanya. Jambo hili linaweza kuleta hasara kwa bwana wetu na jamaa yake yote. Yeye ni mutu mubaya na hakuna anayeweza kusema naye.”


Mufilistini akamwambia Daudi: “Kuja kwangu! Mwili wako nitawapa ndege na nyama wa pori!”


Yawe akasema: “Watu hawa ni taifa moja na wote wana luga moja; huu ni mwanzo tu wa yale watakayofanya. Jambo lolote wanalokusudia kufanya watafanikiwa.


Na kama mutu huyo akimujibu: “Ngojea kwanza niteketeze mafuta halafu utakamata kadiri unataka”, hapo huyo mutumishi wa kuhani anamujibu: “Hapana, unapaswa kunipatia sasa hivi. Kama sivyo, nitaitwaa kwa nguvu.”


Kosa la dada yako Sodoma, lilikuwa hili: yeye pamoja na wabinti wake walipokuwa na chakula nao walifanikiwa sana, walianza kujivuna, wakaacha kuwasaidia wamasikini na wakosefu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite